Christian Churches of God

[134]

 

 

 

Yoshua, Masihi,

Mwana wa Mungu

 

(Toleo La 3.0 19950909-20000219)

 

Jarida hili linaelezea kuhusu ni nani anayepasaswa kuabudiwa kwamba ni Eloa. Mwana ambaye alikuwa ni elohim wa Israeli na Yoshua Masiahi ananyeshwa kwenye muktadha sahihi wa kibiblia. Matumizi ya jina Yoshua kwenye Biblia kumeelezewa na kuainishwa pia.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki Hati © 1995, 1996, 1998, 2000 Wade Cox)

 (Tr. 2017)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:

http://www.logon.org and http://www.ccg.org

 

 


Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu



Kumbukumbu la Torati 6:4-5 Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako 

 

Andiko hili ni Shama au Shâma´ (SHD 8085). Jina lenyewe limechukuliwa kutoka kwenye neno Shama linalomaanisha kusikia ambalo ni neno la kwanza kwenye andiko hili. Ukanunishaji wan eno kusikia maana yake ni kusikia na kuelewa. Man no yenyewe yamechanganyika kati ya Kirumi na Kiebrania:

Shama Y’srael Jehovah Elohinu Jehovah Ehad
Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.

  

Neno Mungu lililotumiwa kwenye tafsiri ya Kiingereza God limeeleweka kwa ujumla kama lilivyotafsiriwa kwenye kamusi ya SHD 430 elohim. Hatahivyo, elohim ni neno la uwingi, ambalo laweza kutumika pia kwenye umoja. Neno la umoja katika kumtaja Mungu na neno lililosahihi zaidi linalofanana au kuhusiana na neno hili ni la umoja Eloah. Andiko lililo kwenye Kumbukumbu la Torati 6:5 linaenda mbali zaidi kwa kutumia kijisarufi chanya kwenye jina Yehovah Eloheik lenye maana ya Bwana Mungu wako. Kumbukumbu la Torati 6:3 inatumia neno YYehovah Elohi kama Mungu wa Mababa. Haya ni maandiko yanayomtaja kiumbe mmoja lakini Elohi anaonenaka kwa kisarufi cha uwingi. Elohim ni neno la uwingi. Eloah ni neno la umoja linaloonyesha kuwa hakuna uwingi. Eloah ni Mungu Baba kutokana na Mithali 30:4-5 aliye na mwana. Wale wateule wanao lijua hilo wanaweza kulitangaza jina lake.

 

Mungu huyu, Eloah, ni Mungu Aliye Juu Sana. Mungu huyu Aliye Juu Sana hakai kati ya watu (Matendo 7:48). Sisi tu watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana (Matendo 16:17) ambaye ameonyeshwa na kutambulishwa kwenye Agano la Kale kama Mungu wa Mababa wa Imani. Hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu huyu wala kumsikia sauti yake (Yohana 1:18; 1Timotheo 6:16).

 

Jina la Bwana kwenye Agano la Kale ni Eloah. Ezra anaonyesha kwamba Eloah ni Mungu wa Hekalu, ambaye nyumba ile ya ibada iliwekwa wakfu kwake. (Ezra 6:16-17), na ndiye aliyekusudiwa kuabudiwa humo (Ezra 4:24; 5:1-2,5,8,13-16; 6:7-8) huko Yerusalemu (Ezra 5:17; 6:5). Eloah ni Mungu wa mbinguni na duniani (Ezra 5:11; 6:9). Dhabihu zinatolewa kwa Eloah wa mbinguni (Ezra 6:3, 10). Alikuwa ni huyu Eloah  aliyesababisha jina lake likae huko Yerusalemu (Ezra 6:12). Makuhani wamepangiwa kwenye maeneo yao chini ya kuhani mkuu na Walawi kwenye maeneo yao waliyopangiwa kuhudumu ili kumtumikia Eloah (Ezra. 6:18) (soma pia jarida la Mungu Tumuabuduye (Na. 002)).

 

Eloah ni Mungu aliye Muumbaji na ni Mwamba wa wokovu. Yeshuruni alimtafuta Eloah aliyemuumba na alikuwa ni Mwamba wa wokovu wake (Kumbukumbu la Torati 32:15) na alitoa dhabihu kwa mapepo ambao hawakuwa Eloah au walengwa stahiki wa kuabudiwa (Kumbukumbu la Torati 32:17). Ni Eloah peke yake ndiye anayestahili kuabudiwa mle Hekaluni. Ndiye anayestahili anayeonekana kuwahudumia Wana wa Mungu kwenye kitabu cha Ayubu. Jina Eloah linajitokeza mara 45 kwenye kitabu cha Ayubu. Eloah hajawahi kuwa na makala (ingawaje limeandikwa kwa kisarufi kwenye Habakuki 1:11, na linaonekana mara moja tu kwenye auandishi wa Zaburi 114:7; Marvin H Pope El in the Ugaritic Texts; soma pia ‘eloah, R. Laird Harris et al., Theological Wordbook of the Old Testament, Moody Bible Institute, Chicago, 1980, p. 43). Eloah halijawahikuonekana likijumuishwa na jina linguine takatifu (ibid.).

 

Eloah anajulikana na kuonyeshwa kama Mungu aliyefunuliwa kwenye Kutoka 34:6-7 kama tunavyoona kutokana na matumizi yake kwenye Nehemia 9:17.

Kutoka 34:6-7 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; 7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne. 

 

Kwa hiyo Yahova aliyekuwa akipita mbele ya Musa akimtangaza El ambaye alijulikana kuwa ni Eloa alikuwa Mungu.

Nehemia 9:17  ila wakakataa kutii, wala hawakuyakumbuka maajabu yako, uliyoyafanya kati yao; lakini wakafanya shingo zao kuwa ngumu, na katika kuasi kwao wakaweka jemadari, ili wairudie hali ya utumwa; lakini wewe u Mungu, uliye tayari kusamehe, mwenye neema, mwenye huruma nyingi, si mwepesi wa hasira, u mwingi wa rehema, basi hukuwaacha.

 

Danieli 11:37-39 inaonyesha kuwa mpingamungu mkuu alikuwa mungu au eloah, aliyejiimarisha mwenyewe. Kwa hiyo Eloah anaonekana kama Mungu sahihi na anayefaa na kustahili kutumainiwa. Jina Eloah lina maana sawa tu na jina Elah[h] jina analoitwa \Mungu kwa Kiaramu kilichotumika kwenye biblia. Mungu huyu ni Mkuu na Muweza kama tunavyoona alivyotumika kwenye Ayubu. Eloah ni msingi au chimbuko la jina la All’ah wa Waislamu.

 

Jina Eloah limejitokeza mara tatu kwa sambamba na neno mwamba kama neno lisiloloelezeka kuhusu Mungu (Kumbukumbu la Torati 32:15; Zaburi 18:31 [H 32]; Isaya 44:8). Kwa ujumla, kwa uchache Eloah limetumika mara tatu kwa muktadha wa utisho kwa wenye dhambi (Zaburi 50:22; 114:7; 139:19). Mlengwa akiwa ni Eloah, Baba, alikuwa ndiye muumbaji na anayeuongoza na kuufanya uwepo ulimwengu (Mwanzo 1:1; Nehemia 9:6; Zaburi 124:8; Isaya 40:26,28; 44:24; Matendo 14:15; 17:24-25; Ufunuo 14:7). Kwa utashi wake vitu vyote vilumbwa na kuwepo.

Ufunuo 4:8-11 Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; na pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja. 9 Na hao wenye uhai wanapompa yeye aketiye juu ya kiti cha enzi utukufu, na heshima, na shukrani, yeye aliye hai hata milele na milele, 10 ndipo hao wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi, nao humsujudia yeye aliye hai hata milele na milele, nao huzitupa taji zao mbele ya kile kiti cha enzi, wakisema, 11 Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.

 

Mlengwa huyu kwenye ibada ya Mwanakondoo na baraza la Wazee ni Mungu ambaye ndiye Baba. Baraza la Wazee ni serikali ya mbinguni ya Mungu.

 

Mungu kabla ya mwanzo

Mungu alikuwepo na aliishi peke yake kabla ya kiukmbe kingine chochote. Alikuwa peke yake kabla ya mwanzo wa uumbaji. Hivyo, ni yeye peke yake ndiye alikuwepo kabla ya kuwepo kwa vitu vote.

Isaya 43:10  Ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine.

 

Kabla ya yeye hakuna El aliyekuwepo wala aliyeumbwa na wala hatakuwepo mwingine baada ya yeye na aliye kama yeye. Kwa hiyo, yeye ni wa Kwanza na wa Mwisho, Alfa na Omega. Kutokana na Ufunuo 1:8, ufunuo ambao Mungu alimpa Yesu Kristo, Mungu anamwambia Kristo kwamba yeye ni Alfa na Omega na ni Mwenyezi.

 

Ufunuo 1:8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.

 

Hivyo basi, Baba akiwa ni Eloah, ni Mwenyezi na ndiye mwanzo wa uumbaji pamojja na uumbaji wake. Anaanikiza uweza huu kwa Masihi kwa ujio wake (Ufunuo 22:13). Jambo hili limeainishwa pia kwenye jarida la Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229)).

 

Ushirikishaji wa Eloah kwa Elohim kama muundo wa uwingi pia unaonekana kiashirio kwenye matumizi ya jina Yahova (Kamusi ya Strongs Hebrew Dictionary (SHD) 3068) na Yahovih (SHD 3069). Kuna viumbe wengi wanaojulikana na kuitwa jina hili la Yahovah, (pia wanaitwa Yehova au Yahweh kwa wengine) kwenye Agano la Kale. Yahovah anajulikana kama Mungu wa kitaifa wa Israeli na anajulikana kama Adonai na Wayahudi wanapolisoma jina lake. Yehovih anajulikana kama ni Mungu na anaitwa elohim na Wayahudi wanapokuwa wakiyasoma maandiko. Viumbe wawili wanahusishwa. Na hii ndiyo maana Yahovah alibadilishwa kuwa Adonai mara 134 kwenye Agano la Kale na baraza la Sopherim. Yahovah ni jina la kicheo lililotolewa linaloainika kwa viumbe wengi kama ilivyokuwa kwa suala wakati Yahovah watatu walipojitokeza na kunena na Ibrahimu kabla ya kuangamizwa kwa Sodoma na wawili kati yao walikwenda kwa Lutu huko Sodoma. Kulikuwa na Yahovah wa nne Mbinguni waliounyeshea moto mji wa Sodom (soma Mwanzo 19:24). Maandiko haya yalibadilishwa na baraza la Sopherim (kwa mujibu wa The Companion Bible, Appendix 32; na soma pia jarida la Mkururu wa Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara 1: Asili ya Mungu (Na. 003)).

 

Swali lote la mwanzo wa nyakati limeainishwa kwenye jarida la Serikali ya Mungu (Na. 174). Kuna wakati ambapo Roho alikuja kuwa na uhusiano na siyo kwa kushirikishwa kwenye mamlaka ya kimungu kama mbadala wa Mungu. Mungu alikuwepo kuwa ni wa milele. Ni yeye tu ndiye hafi wala kupatwa madhara (1Timotheo 6:16). Mungu ni mfalme na Bwana wa nyakati zote (1Timotheo 1:17; sawa na yasemavyo maandiko ya Kiyunani ya Tobiti 13:6,10) na Mungu wa nyakati zote (theos tõn aiõniõn, sawa na Ecclus. 36:17; Isaya 9:6; Yeremia 10:10). Harakati za uumbaji wa Mungu ulianzisha udugu wa Roho kuweka nyakati. Mungu alianikiza uweza wa kuwa asiyeweza kufa wala kupata madhara kwa wana wa Mungu tangu kuumbwa kwao. Kwa uumbaji wa mwenendo huru au wa kujitegemea kwa Roho, kama mwingiliano wenye weledi mkubwa wa Mungu, zama zikaanza.

 

Mwanzo

Mungu alianza kuumba. Tendo la kwanza la uumbaji, kwa uzao lilikuwa ni kumhuluku Mwanae aliyemfanya elohim. Huu ulikuwa ni uumbaji wa kiroho. Hawa wana wa Mungu walikuwa ni wengi. Roho Mtakatifu alikuwa ni uweza au kiini chimbuko takatifu na nguvu iliyowaunganisha elohim hawa wawili na ambaye aliwawezesha kuwa wamoja na Mungu (soma majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117)Uzima wa Milele (Na. 133)Kufanyika Sawa na Baba (Na. 081); Jinsia ya Roho Mtakatifu (Na. 155)Manabii Wajumbe wa Mungu (Na. 184); Mungu Mwokozi Yetu (Na. 198)). Nyakati zilianza kwa kuumbwa kwa Jeshi la Malaika (soma pia kitabu cha Augustine cha Mji wa Mungu; na jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)).

 

Baraza la Hawa Elohim Kama Wana wa Mungu

Wana wa Mungu walihisishwa kwenye muundo huu. Waliongozwa na Baraza, ambalo limeonekana kwenye Kitabu cha Ufunuo. Linajumuissha viumbe ishirini na tisa wanaokizunguka kiti kitukufu cha Mungu. Kuna wazee ishirini na walio chini ya kuhani mkuu. Kuna pia maserafi (wanaoitwa viumbe wenye uhai kutokana na jinsi vichwa vhao vinavyoonekana). Shetani alikuwa ndiye yule Kerubi afunikaye kwenye Kiti cha Enzi cha Mungu (Ezekieli 28:14).

 

Baraza hili linaitwa Baraza la Elohim au Baraza la Mungu na Viumbe wengine wateule wa Mbinguni. Uumbaji halisi ulifanywa na elohim.

Mwanzo 1:1  Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

 

Dunia ilikuwa bado ingali tupu haina kitu. Giza lilitanda juu ya uso wa vilindi na Roho wa Mungu alituama juu ya uso wa vilindi vya maji (Mwanzo 1:2).

 

Huyu elohim ndiye aliyemuumba mwanadamu kwa sura na mfano wa elohim baada ya kufanana na wao.

Mwanzo 1:26-27 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.  

Hapa elohim anapanga mkakati wa kumuumba mwanadamu (adamu pasipo kutumia zana wala kiambata chochote; akafanyika kuwa binadamu) kwa sura na mfano wake. Aya ya 27 ndipo inapunguza idadi kwa umoja vile aliyeumba. Mtu aliyeumbwa hapa ni adamu kwa kiambata, na ndiye Adamu. Kwahiyo kuna mambo mawili kwenye uumbaji huu.

 

Kwahiyo uumbaji imefanywa kotekote, yaani mbinguni na duniani (Mwanzo 2:1). Tunajua kutokana na Kumbukumbu la Torati 32:8-9, kwamba Mungu Aliye Juu Sana aliyaanzisha mataifa sawasawa na Wana wa Mungu (bene Eliym; DSS) au malaika wa Mungu (‘agellon theou; LXX). Mandiko ya Masoretic yalibadilishwa, wakati fulani baada ya Kristo, kuyasoma kwa mujibu wa idadi ya Wana wa Israeli.

Kumbukumbu la Torati 32:8-9 Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, Alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli. 9 Maana, sehemu ya Bwana ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake. 

 

Tafsiri ya RSV inakubaliana na andiko sahihi kwenye tafsiri yake. Kulikuwa na Wana wengi wa Mungu (soma pia jarida la Uwepo wa Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243)).

 

Nyota za Mungu

Mungu Aliye Juu Sana anajulikana kama Baba na muumbaji, kutokana na Kumbukumbu la Torati 32:6.

Kumbukumbu la Torati 32:6-7 Je! Mnamlipa Bwana hivi, Enyi watu wapumbavu na ujinga? Je! Yeye siye baba yako aliyekununua? Amekufanya, na kukuweka imara. 7 Kumbuka siku za kale, Tafakari miaka ya vizazi vingi; Mwulize baba yako, naye atakuonyesha; Wazee wako, nao watakuambia.

 

Kwahiyo, Mungu Aliye Juu Sana ni Baba na Wana wa Mungu ni wazee. Yahovah aliye kwenye andiko hili ni mshirika wa Mungu wa Israeli. Kwa hiyo, jina Yahova ni mamlaka yaliyotokana na Mungu Aliye Juu Sana ambaye ni Baba. Aliwafanya elohim na kuwaweka kwenye mataifa sawasawa na idadi yao, ambayo kwa kweli ni sabini. Kuna Mabaraza yote mawili ya Wazee au Elohim, ambayo ni la ndani na la nje. Yahova amewekwa aketi kwenye Baraza hilo. Alitiwa mafuta kuwa Mungu wa Israeli ili kuanzisha mpango wa wokovu wa Mungu, ambao ulikuwa ni wa muhimu kutoka kwenye Bustani ya Edeni na uasi wa Malaika, wakati Shetani alipowekwa kwenye Bustani ya Edeni awe kama Kerubi au     Nyota ya Asubuhi au Nyota ya Siku au ya Mchana (soma jarida la Fundisho la Chanzo au Chimbuko la Dhambi Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246)).

 

Cheo cha Nyota ya Asubuhi kilikuwa cha wengi tangu uumbaji na kimeainika hadi kwa Kristo na kwa wateule.

Ayubu 38:4-7 Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu. 5 Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? 6 Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, 7 Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?  

 

Kulitakiwa kuwe na nyota inayotoka kwa Yakobo kwa mujibu wa Hesabu 24:17. Hii ilitakiwa kuchukua nafasi ya ile nyota iliyoanguka kutoka mbinguni (Ufunuo 8:10). Hii inamwashiria Kristo aliyechukua mahali pa Shetani kama Nyota ya Asubuhi (soma pia jarida la Lusifa: Mpeleka Nuru na Nyota ya Asubuhi (Na. 223)Kusudi la Uumbaji na Dhabihu ya Kristo (Na. 160); Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229)).

 

Nyota ya Siku au Nyota ya Asubuhi inapambazuka mioyoni mwetu (2Petro 1:19). Tumepewa huyu Nyota ya Asubuhi kwa kupitia Kristo (Ufunuo 2:28; 22:16). Wote ni wadogo na wasaidizi kwa Mungu Aliye Juu Sana.

 

Mwana ambaye ndiye alikuwa Elohim wa Israeli

Israeli waliuelewa uhusiano huu wa aliye mkubwa na bora na aliye mdogo na elohim msaidizi. Iliaminika na kujulikana kuwa Baba ndiye aliye Bora na Mkuu zaidi au ni Mungu Aliye Juu Sana. Alikuwa pekee kama Eloah, El wa El. Mwana wa Mungu aliyetiwa mafuta awe kama Yahovah au Elohi wa Israeli alikuwa mdogo.

Zaburi 45:6-7 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 7 Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.

 

Anayenenwa hapa ni Elohim wa Israeli tunayemjua leo kama Yesu Kristo.

Waebrania 1:8-9  Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

 

Kipindi chote cha hadi kuzaliwa kweke Yesu Kristo hapa Duniani, cheo chake kilikuwa ni kama mmoja wa hawa elohim tu, na alipokuwa anatenda jambo lolote, nao walionekana kuwa walikuwa wakifanya vivyohivyo. Aliinuliwa juu zaidi kuliko wenzake wengie wote kwa kufufuka kwake kutoka mautini akiwa kama Mwana wa Mungu mwenye uweza kwa kupitia Roho Mtakatifu.

Warumi 1:4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu; 

 

Uwingi huu wa hawa elohim unaonekana kwenye fafanuzi za Wafilisti.

1Samweli 4:8  Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa na mkono wa miungu hawa walio hodari? Hawa ndio miungu waliowapiga Wamisri kwa mapigo ya kila namna jangwani.

 

M8iungu hawa wenye nguvu wanaotajwa hapa wanaonekana moja kwa moja kuwa ni elohim wenyewe. Kwa hiyo, Yahovah aliwaambia hawa elohim. Mwana wa Mungu kwenye jeshi la Israeli alitenda kazi kwenye mamlaka na sambamba na Baraza ambalo walikuwa ni washirika wake (metoxous Zaburi 45:6-7 LXX; Waebrania 1:8-9). Mataifa yalielewa pia uwingi huu wa hawa elohim.

1Wafalme 20:10  Ndipo Ben-hadadi akatuma kwake, akasema, Miungu wanifanyie hivi na kuzidi, yakiwa mavumbi ya Samaria yatatosha makonzi ya watu wote walio miguuni pangu.

 

Miungu inayotajwa hapa ni elohim. Kwa hiyo Ben-hadad alimjua huyu elohim.

 

Yahovah wa Israeli anatoa hukumu katikati ya elohim.

Zaburi 82:1  Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu.

 

Hapa, elohim amechukua mahala pake kati ya miungu au El. Katikati ya hawa elohim anatoa hukumu. Andiko linaendelea kwa kuainikiza Uwana huu kwa Jeshi lote la malaika. Kama tujiavyo, huyu ilieleweka kama mteule na Irenaeus (soma jarida la Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127)).

Zaburi 82:6  Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.

 

Miongoni mwa elohim ilichukuliwa kuwa hakuna aliye kama Yahovah (Yehova) (aliyetafsiriwa hapa kama Bwana).

Zaburi 86:8  Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.

 

Yoshua au Yesu Kristo wa Agano Jipya

Ni muhimu sana kwamba tunajua hiyo inatokea kwenye Agano Jipya na mahali jina Yesu linapotokea na kile ambacho matumizi yake yanakusudiwa kumaanisha.

 

Yesu halikuwa jina la Yesu Kristo, yaani Masihi. Jina lake lilikuwa  ni Yoshua au Joshua kwa matumizi ya Kiingereza, ambalo siyo kwa J ya mkato, bali ni matamko ya J laini. Jina la Joshua limekuwa hivyo mara kwa mara kwenye matumizi ya Kiingereza kwa kipindi cha maelfu ya miaka. Linaonekana kidodoso kwenye Agano la Kale na kwenye sura kadhaa za Agano Jipya. Kiyunani cha Agano Jipya kinatumia miundo ambayo ilikutikana kwenye tafsiri ya Septuagint ya Maandiko Matakatifu ya Kiebrania, ambayo yalitafsiriwa huko Alexandria yapata miaka takriban mia tatu kabla ya Kristo.

 

Maandiko Matakatifu ya Septuagint yalikuwa na malengo yaliyofikiwa yenye maana sana. Yana kiwango mwanana cha aina ya Kiyunani chenye maneno ya Kiebrania. Ièsous ni jina la Kiyunani la kwenye tafsiri ya Septuagint lenye maana ya neno Yoshua au Joshua kwenye Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale. Septuagint ilikuwa ni Biblia ya Agano Jipya. Nukuu nyingi zilizonukuliwa kwenye Agano Jipya zinatokana na tafsiri hii ya Septuagint (LXX). Septuagint ilikubalika kuwa ni Maandiko Matakatifu wakati wa Kristo. Ililaumiwa na kuonewa mashaka na Mafarisayo kipindi cha baada tu ya kuangamizwa kwa Hekalu, na kutotumiwa au kuchukiwa na marabi, baraza lililofanyika hatimaye kuwa ni warithi jopo la Kifarisayo, kipindi cha baadae yapata kama kwenye karne ya pili hivi.

 

Kwa hiyo, wakati wa Kristo kulikuwa na mabishano kuhusiana na Septuagint kuwa kama ni Maandiko Matakatifu ama la. Kwa kweli inaweka misingi ya Agano Jipya. Maneno ya Kiyunani kwenye Septuagint yalitumika kwa majina ya tabia na mwenendo wa Kanisa la Agano Jipya na kwamba Kiyunani hatimaye kilitafsiriwa kwa Kiingereza kipindi cha baadae sana. Karne nyingi zilizofuatia ziliendeleza kuandikwa kwa tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza za Agano Jipya.

 

Sasa tatizo likuwa kwamba, neno Yoshua lilitafsiriwa kutokana na neno la Kiyunani ambalo liliandikwa Joshua, ambalo linajitokeza mara nyingi kwenye Agano Jipya, na linahusiana na idadi kadhaa ya watu mbalimbali na limetafsiriwa kwa namna nyingi mbalimbali. Kwa mfano, kwenye tafsiri ya KJV, Waebrania 4:8, neno lililotumiwa la Joshua lilitafsiriwa kama Jesus (Yesu) mara nyingi sana, na kufanya kwamba lionekane neno Yoshua na kwenye Agano Jipya lote lisomeke Yesu kutokana na neno la Kiyunani la Ièsous kuhusu Yoshua. Lakini Waebrania 4:8 inamtaja Yoshua mwana wa Nuni na ndivyo linavyojulikana na Biblia nyingine zote zinapomtaja Yoshua mwana wa Nuni. Bullinger kwenye uandishi wake wa Companion Bible anakubaliana kwamba Waebrania 4:8 haikusudii kumtaja Yesu, kwa maana ya kuwa ni Kristo, bali inakusudia kumtaja Yoshua mwana wa Nuni.

 

Yoshua mwingine aliyeitwa Yusto kwenye Wakolosai anaitwa pia kuwa ni Yesu aitwaye Yusto (Wakolosai 4:11). Kuna mionekano mingine na kutajwa kwa Kristo kwenye mistari ya uzao wa Yesu. Kwenye Luka 3:29 tunasoma kwamba Yoshua huyu alikuwa ni mwana wa Eliezeri. Sasa neon hili lililotafsirwa Yoshua ni neno la Kiyunani la Yoshua anayeitwa Yesu. Hakuna andiko linalomaanisha kikamilifu sana kwa mba Yoshua mwana wa Eliezeri na baba wa Eri ni kwa hakika anaitwa Yesu. Hii ni kwa sababu tu kwamba ni namna ya kuandika kwa Kiyunani kwa jina Yoshua kwa kutumia kanuni iliyoanzishwa kwenye Septuagint. Tafsiri ya KJV inaubadilisha au kuugeuza ukweli huu kwa kumtaja Yoshua hapa kama Yose. Kanuni hii ya Kiyunani inayoandika Yoshua inafuatiwa kwenye Waebrania 4:8 na mahali penginepo. Kuna mtu mwingine ambako limetumika neno Ièsous na limetafsiriwa kama kitu fulani tena. Kina Yoshua wengi mbalimbali wameandikwa kwenye maandiko wakiitwa Jahoshua (au Yahoshua) na pia Yeshua, Yeshuah, Hosea, Hoshea, Osea lakini tofauti zilifanywa pia kwenye Kiebrania.

 

Matumizi yenye kulinganishwa kwenye nakala ya Septuagint yanaonekana kutoka kwenye jaribio la kila mfano wa neno Yahoshua au Yahshua kwenye Kiebrania cha Agano la Kale na ambapo imechukuliwa hivyohivyo kwenye lugha ya Kiingereza likijulikana kama Joshua. Kwenye kila mfano, neno Yoshua limechukuliwa kama Yesu au Ièsous kwenye Kiyunani. Neno Yesu ni tafsiri ya Kiyunani na siyo sahihi kulichukulia kama lilivyo kama jina lilivyo kwenye lugha ya Kiingereza kwa maana hiyohiyo. Ukweli wa mambo ni kwamba neno Ièsous ni la Kiyunani linalomaanisha Yoshua na unapotafsiri Kiyunani kwenda kwenye lugha ya Kiingereza kwa kuyatumia Maandiko Matakatifu ya Kiebrania, ndipo Septuagint inaunda kanuni. Kanuni ya majina ni kwamba imetumika kwenye kwenye maana iliyokubalika ya Kiingereza, ambapo Maandiko ya Kiebrania yametafsiriwa kwenye lugha ya Kiingereza.

 

Kwa hiyo wakati neno Ièsous linaonekana kwenye Agano Jipya kwa kanuni na uandishi wa Septuagint, linamaanisha Yoshua, ambalo limekuwa ni kigezo mizania cha jina kwa karne kadhaa sasa. Wanazuoni waamini Utatu walipokuwa wakitafsiri toleo la KJV kwenye lugha ya Kiingereza, walijaribiwa kuweka tofauti kati ya Agano Jipya na Agano la Kale na kuondoa uhalisia na watu kwenye Agano Jipya kutoka kwenye Agano la Kale ili kwamba muendelezo wa Agano Jipya na Agano la Kale ubadilike. Hivyo mgawanyiko ulijitokeza kati ya kanuni kama imetokana na Biblia. Sheria au Torati ya Mungu kwenye Agano la Kale ilifanywa kuwa ni tofauti na kile kilichokuwa kikitokea kwenye tukio la Mashihi (Tukio la Kimasihi la Yoshua, Masihi kwenye Agano Jipya). Hivyo walimuita Yesu Kristo ambalo maana yake ni Yesu Mtiwa Mafuta. Yoshua Masihi maana yake ni Yoshua Mtiwa Mafuta. Kwa hiyo neno hili kama linavyoonekana kumhusu Mtiwa Mafuta linamlenga kwenye lugha ya Kiingereza kwenye Agano la Kale Masihi na walikuwepo wengine wengi zaidi ya Masihi mmoja.

 

Kwa hiyo Yoshua ni jina sahihi a huyu Ièsous kwa Kiyunani, ambapo bila shaka kwenye muundo wa kifonetikali, unaoweza kumtaja ukimaanisha kwa muundo wa Agano Jipya na bila shaka unapokuwa unasoma Agano la Kale bado utakuwa unasoma (au unaweza kusoka) Yoshua kama ni Ièsous pia kwa kumaanisha, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyo kwenye tafsiri ya LXX. Hatuna tahshishi na kuongea Kiyunani. Tunahusika na kusema Kiingereza, kwenye tafsiri za Kiingereza tukirejea nyuma kwenye tabia na kanuni za Biblia ili kwamba kuna muundo sahihi, uliowazi na endelevu unaoendelezwa, na Agano Jipya halijajitenga na Agano la Kale.

 

Kuna Biblia moja tu, inayojitosheleza kikamilifu sana kwa mamlaka na inayoshabihiana pasi kupingana. Ni muhimu sana kujua kwamba wakati Biblia inapotafsiriwa kwenda kwenye lugha zingine, kwamba mambo muhimu yaliyo kwenye Agano Jipya pamoja na majina hayo yatafsiriwe kwa namna iliyo sahihi zaidi. Na kwamba yabebe majina ambayo tabia na uhalisia ambao wahusika walikuwanayo kwenye Agano Jipya pamoja na majina hayo yawe yametafsriwa kiusahihi zaidi. Ndipo hatimaye wanayasikia majina kwamba sifa hizo za walengwa zilikuwemo kwenye Agano la Kale kwenye lugha ambayo imetafsiriwa kwayo; hata kama ni Kirusi, Kiukraini, Kifaransa, Kijerumani, Kidachi, au kwa lugha nyingine yoyote ile. Na kwa kweli ni makosa na siyo sahihi kufanya tofauti hizi na hailengi kusudio lolote la msingi, zaidi ya lile la kuipa mashiko na kuisaidia imani potofu ya Utatu na mafundisho potofu ya teolojia ya ki Antinomia ambayo yalikuwa ni kisababishi kikubwa cha tafsiri hizi za kijanja kwa mahala pa kwanza. Ni muhimu kwamba tunafanya marejesho ya kusudio halisi na muundo wa Maandiko Matakatifu.

 

Yoshua lilikuwa jina la Kristo Masihi, kwa kuwa linamaana ya Wokovu wa Mungu. Yoshua mwana wa Nuni aliitwa Wokovu wa Mungu, Mwana wa uvumilivu, ikimaanisha kwamba wokovu huja kwa uvumilivu. Maana ya jina la Masihi yalikuwa ni Wokovu huja kama Mwana wa Mungu. Wokovu wa Mungu unatoka kwa Mungu. Na hii ndiyo maana iliyopelekea Masihi aitwe Yahoshua ua Joshua kwa Kiingereza na sababu jina Yesu aliudhihirisha ukweli huo.

 

Kwa mfano unaposhughulikia suala la mama wa Masihi, tunaona kwamba jina lake lilikuwa ni Mariam na jina lake ni Mariam wakati wote kwenye Agano Jipya lote. Jina la mdogo wake lilikuwa ni Maria. Kwa hiyo jina Mary siyo jina linalojitokeza kabisa kwenye Agano Jipya. Ni upotofu tu uliofanywa na Waanglikana walioweka jina hili la Maria na huyo Maria hakuwa mama wa Kristo kabisa. Kwenye kila mfano isipokuwa mmoja tu, ambapo kuna tofauti fupi sana kumetumika Mariamu ambalo ndilo jina la mama yake na Maria ni jina la shangazi yake. Baba yake alikuwa Yusufu. Tunajua hivyo. Hawakupata shida kuhusu yusufu, lakini wanawaelezea ndugu wa Kristo, badala ya kujataja majina ya kawaida kwa Kiingereza kuhusu hawa ndugu zake, wanawaficha na kuwageuzia mbali.

 

Mambo haya yapaswa yajulikane. Tutayaelezea kwa kina kwenye utangulizi wa kitabu cha fafanuzi kuhusu Biblia na hususan kwenye Agano Jipya wakati tutakapoyachambua majina na kuyaelezea kwa ufafanuzi wa kina matumizi yake. Haionyeshi maana nzuri kuendelea kufanya nadharia upotoe uliopo kwenye uanzishwaji wa kanisa la mrengo wa  Kitrinitarian la Kiingereza, kwamba limefanya uharibufu mkubwa zaidi kwenye uelewa wa Teolojia ya Biblia na Sheria za Mungu, kuliko taasisi nyingine yoyote ile kwenye ulimwengu wa watu wanaoongea lugha ya Kiingereza. Kristo angewakataa na atawakataa kabisa na kuwaona kuwa ni wazushi wa kimafundisho na wapotofu. Hii haimaanishi kwamba tuufuate upotofu wao. Ukweli wa Biblia yapaswa urejeshwe kiuwazi sana na kikamilifu sana.

 

Mungu wa Miungu

Bwana ndiye El Mkuu na ni Mfalme juu ya elohim wote.

Zaburi 95:3  Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu, Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.

 

Elohim wa mataifa anachukuliwa kuwa si kitu (ametafsiriwa kama kinyago au sanamu).

Zaburi 96:4-5  Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote. 5 Maana miungu yote ya watu si kitu, Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.

 

Bwana anayetajwa hapa ni Yahovah aliyeinuliwa juu kuliko elohim wote. Jambo hili linaibua mambo fulani ya muhimu sana kuhusu Yahovah (Jehovah)  ni kama jina tuliloliona hapo juu.

 

Zaburi 97:7-9  Na waaibishwe wote waabuduo sanamu, Wajivunao kwa vitu visivyofaa; Enyi miungu yote, msujuduni Yeye. 8 Sayuni imesikia na kufurahi, Binti za Yuda walishangilia, Kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana. 9 Maana Wewe, Bwana, ndiwe Uliye juu, Juu sana kuliko nchi yote; Umetukuka sana juu ya miungu yote.

 

Hapa Yahovah anatajwa kama Mungu Aliyejuu sana. Hivyo tunaongelea vitu viwili tofauti, Yahovah wa Israeli na Yahovah Alye Juu sana (au Jehovah) Aliye Juu sana kulik elohim wengine wote.

 

Kuhani Mkuu na Mungu wa miungu

Zaburi 135:5  Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu, Na Bwana wetu yu juu ya miungu yote.

 

Hapa Adonim au Bwana wetu ni yeye aliye juu ya elohim wote. Kwa hiyo mtangulizi aliyepo hapa ameinika kuwa Elohim wa Israeli. Kwa hiyo ameonekana na kufanywa kuwa ni Kuhani Mkuu wa Elohim. Hata hivyo yeye siyo Elohim wa Elohim. Hii imeachwa kwa Eloah au Yahovah Aliye Juu Sana.

Zaburi 136:2  Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.

 

Yeye peke yake ndiye adonim wa adonim au ni Bwana wa Mabwana. Aliunda uwakilishi na hivyo ni uwingi wa andiko lililo kwenye Yeremia 10:10-11.

Yeremia 10:10-11  Bali Bwana ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake. 11 Mtawaambia hivi, Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu. 

 

Kuna Mungu mmoja tu wa kweli kama tunavyoona. Yeye ni Mungu aliyehai na ni mfalme wa milele. Hawa elohim wana majukumu mbalimbali kwenye uumbaji. Mungu mmoja, wapekee na wa kweli aliiumba dunia kwa uweza na hekima yake.

Yeremia 10:12-13  Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.13 Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake. 

 

Tendo hili la uumbaji lilifanywa kwa utadi mkubwa na Mungu. Majukumu mengine ya uumbaji yalibebwa na Masihi, mzaliwa wa kwanza wa uumbaji. Hata hivyo, jukumu na jambo moja linahitaji ufafanuzi.

Waefeso 3:9  na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;

 

Maneno ya dia ‘Iesou Christou au kwa Yesu Kristo hayako sahihi. Maneno haya yapo kwenye tafsiri ya Receptus na kisha kwenye KJV lakini hayajitokezi wala kuonekana kwenye maandiko ya zmani. Hayaonekani kwenye tafsiri za kisasa za Biblia. Tafsiri ya RSV kiusahihi zaidi inaandika andiko hili kama h9ivi:

Waefeso 3:9  na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;

 

Wakolosai 1:15-20  naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. 18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. 19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae; 20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.

 

Tazama jinsi inavyosema yeye ni mwanzo (yani Khristo).

 

Muundo wa kiuongozi wa utaratibu wa kidini haupaswi ukanganywe na viumbe wa elohim wenyewe. Huyu wa kale anayetajwa hapa kwenye Wakolosai amekusudiwa kwenye kuyashinda malumbano yanayohusu uumbaji wa ulimwengu kwa kupitia suala ambalo lenyewe tu lilichukuliwa kuwa ni wakale (soma kwenye majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117); na Mwendelezo wa Mtindo wa Kiplatoniki Mamboleo (Na. 017)).

 

Ilikuwa ni kizazi cha Kristo na wana wa Mungu ambacho kilikuwa ni cha mwanzoni mwa uumbaji wa Mungu. Mwanzo huo wa uumbaji wa Mungu ndiyo unaomaanishwa kwenye Ufunuo 3:14.

 

Katika Kristo utimilifu wote wa Mungu ulipendezwa uwepo. Kwa hiyo, Kristo ni kifaa au chombo cha Mungu kama mwanzo wa uumbaji wake. Alikuwa ni mzaliwa wa kwanza katika wafu ili kwamba kwenye vitu vyote aweze kuwa kwenye mahali pa kwanza. Hata hivyo, vitu vyote vina Baba mmoja na chanzo kimoja na muumbaji mmoja ambaye kwa yeye tu peke yake ndiye Mungu mmoja, wapekee na wa kweli.

Malaki 2:10  Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu?

 

Huyu Baba ndiye Bwana wa Majeshi (Malaki 1:6). Anaanikiza nafasi ya Ubaba kwa elohim kwa kuwapa mamlaka. Isaya 9:6 inaendelea kuanikiza Ubaba huu kwa Masihi. Kuna aina nyingi za Ubaba au mababa (Patria) mbinguni na hapa duniani na wamejulikana na kuitwa Mababa (Waefeso 3:14).

Waefeso 3:14-15  Kwa hiyo nampigia Baba magoti, 15 ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,

 

Dhana ya Kuzaliwa Hapa Duniani ki Mabadiliko ya Zama Moja Hadi Nyingine Kimaumbile

Waebrania 1:6 inamtaja kiumbe aliye mzaliwa wa kwanza aliyetumwa na kuletwa duniani. Kiumbe huyu, mzaliwa wa kwanza (prõtotokos) wa kila kiumbe anayetajwa kwenye Wakolosai 1:15, ametambuliwa kama Mwana. Mwana ndiye pia prõtotokos wa Mariamu (au Maria) (Mathayo 1:25; Luka 2:7). Huyu Mwana alikuwa pia ni prõtotokos miongoni mwa ndugu wengi. Hivyo basi, jina hili linamaanisha wa kwanza kwenye mkururu ambao unajulikana kama anayestahili.

 

Waamini utatu wengine wanafikia hata kudai kwamba Mariamu (Maria) hakuwa hata na watoto wengine. Huu ni uwongo. Kristo alikuwa na ndugu wengine wengi, wakike na wa kiume (Mathayo 13:55-56); (sawa na lisemavyo jarida la Bikira Mariamu na Familia ya Yesu Kristo (Na. 232)). Majina ya hawa ndugu wa kiume wa Kristo yalikuwa ni Yakobo, aliyeitwa James na Wapagani Yusufu aliyeitwa jina la baba yake, Yuda aliyeitwa jina la kabila lake; na Simeon. Majina ya dada zake yalikuwepo lakini hayakuandikwa, lakini majina haya yako wazi na yanajulikana sana na yanatofautiana na yameandikwa kwenye Kiingereza kutokana na Agano la Kale. Kuna sababu ya muhimu sana na ya wazi kwanini yalibadilishwa. Ilikuwa ni kukusudia kukanusha ukweli wa kwamba Kristo alikuwa na ndugu wengine wa kike na wakiume na ili kumtukuza zaidi Mariamu ili astahili kuongekana kuwa ni mungumke mlengwa wa ibada za Easter na imani hii. Kupinga au kukataa kwamba Mariamu (Maria) hakuwa na watoto wengine ni makosa makubwa wakati inaonekana wazi kwamba kuna mtoto anayeitwa Yusufu mwanawake Mariamu, mmoja wa ndugu wa Kristo, na jina la baba yake aliitwa Yusufu. Ni ukweli ulio wazi sana kwamba alikuwa anaitwa jina la baba yake. Haya ni majina ya kifamilia ambayo unatarajia kuyaona kwenye familia ya Kristo.

 

Masihi hapa ni mzaliwa wa kwanza pia wa wafu. Kwa hiyo yeye ni mwanzo akiwa kama kichwa cha mwili na ushirika huu. Kwa muktadha huohuo alikuwa pia mwanzo wa uumbaji wa Mungu (Ufunuo 3:14). Muundo wote mzima uliwekwa na Mungu kwa kuruhusiwa. Kwa hiyo alikuja ili awepo ili aweze kukamilisha mpango wa Mungu kama ilivyofanyika kwa viumbe wengine wote. Kutanglia mbele kwa Masihi kunapatikana kutokana na mpango wa Mungu na kwa amri ya Mungu (soma jarida la Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229)).

 

Tunajua kutokana na Tunajua kutokana na Yohana 17:3 na 1Yohana 5:20 kwamba Mungu huyu Mmoja, Wapekee na wa Kweli ni Baba na kwamba Yesu Kristo ndiye mwana wake.

Yohana 17:3  Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

 

1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.

 

Mungu huyu mmoja, wa Pekee na wa Kweli ndiye uzima wa milele. Tumepewa uelewa huu na Mwana wa Mungu ili kwamba tuweze kumjua yeye aliye wa kweli na kwamba tuweze kuwa ndani yake yeye aliye wa kweli na ndani ya mwanawake Yesu Kristo au Yoshua Masihi. Mungu huyu mmoja ana uzima wa milele. Ni yeye tu ndiye hafi wala kupatwa na madhara yoyote.

1Timotheo 6:13-16  Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, 14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo; 15 ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana; 16 ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.

 

Ilimpasa Masihi auachiliembali uzima wa milele aliokuwa amepewa na Baba na akakubali kuwa na mwili wa kibinadamu. Aliachilia mbali uzima wake kwa kuamriwa na Baba na akauchukua tena kwa amri ya Baba (Yohana 10:17-18).

Yohana 10:17-18 Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. 18 Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu. 

 

Hivyo, ni Mungu huyu ndiye anayetoa uzima kwenye vitu vyote.

 

Kurudi Mara ya Pili

Kurudi na kuonekana kwa Mwana wa Mungu kumefanywa kudhihirike wazi kwa wakati sahihi na yeye aliye Mkuu wa kipekee ambaye ni Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana nay eye pekeyake ndiye hafi wala kupatwa na madhara (soma jarida Uzima wa Milele (Na. 133) na Kwenye Hali ya Kutokufa wala Kudhurika (Na. 165)). Amemkabidhi Mwana mambo haya ili kuanzisha Ufalme wa Mungu kama tunavyoona kwenye Ufunuo 17:14 na 19:16. Majina haya yameandikwa kwenye kanzu au vazi na kwenye paja la Masihi.

Ufunuo 19:11-16 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. 12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. 13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu. 14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. 15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. 16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA. 

 

Mungu hufanya kazu kwa kupitia Mwana wa Mungu kama alivyomfanya kuwa kuhani mkuu

Neno la Mungu ni Mwana wa Mungu. Huyu Mwana alikuwa pamoja na Mungu hapo mwanzoni. Huyu ndiye alikuwa (au aliendelea) na Mungu (ton theon) na huyu alikuwa ni theos au elohim. Tunajua kuwa huyu elohim ni mdogo (soma Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9). Paulo anakubali kwamba hakuna Mungu mwingine (theos) ila ni mmoja tu; akini kulikuwa na miunguu wengi (theoi) (theoi polloi) na mabwana wengine pia (kurioi) mbinguni, lakini kulikuwa na Mungu mmoja tu aliye Baba na Bwana mmoja Yesu Kristo (1Wakorintho 8:5-6; soma Kamusi ya Marshall’s Interlinear). Kazi na shughuli zote zitakuwa zimewekwa chini ya hawa na utaratibu na huduma zote za Hekalu zitarejeshwa upya, kwa kweli; kote kuwili, mbinguni na duniani.

 

Mungu alichagua kutenda kwa uwakilishi kwa Mtakatifu wake ambaye ndiye aliyemtia mafuta mfalme wa Israeli kama tunavyojionea kwenye Zaburi 89:18-20.

Zaburi 89:18-20  Maana ngao yetu ina Bwana, Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. 19 Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi, Ukasema, nimempa aliye hodari msaada; Nimemtukuza aliyechaguliwa miongoni mwa watu. 20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, Nimempaka mafuta yangu matakatifu.

 

Tafsiri ya RSV inaonekana kuligeuza au kulipotosha andiko hili huenda ni kutokana na mwelekeo wake (soma kamusi ya Green’s Interlinear ili kujipatia maana na maandiko zaidi).

 

Utaratibu wa kimbinguni uliwekwa kwa kufananishwa na ule wa Hekalu la Duniani la Israeli kutokana na maskani, ambalo limefananishwe na Hekalu la Sulemani.

Waebrania 8:5 watumikiao mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema; maana asema, Angalia ukavifanye vitu vyote kwa mfano ule ulioonyeshwa katika mlima.

 

Tunaona pia kwamba kulikuwa na makerubi watiwa mafuta wawili wafunikao, au Makerubi wa kwenye maskani, (Kutoka 25:18-22) waliofunika wawili kwenye Sanduku la Agano. Kerubi pia walijumuisha wenye uhai wanne. Hata hivyo, walikuwepo wawili tu, Kerubi mwenye kichwa cha mwanadamu na kerubi mwenye kichwa cha simba, kwa upande wa nje ya Hekalu la nabii Ezekieli kwa ama upande wa mti wa Mtende ambaye ni Kristo (Ezekieli 41:19). Shetani aliwekwa pamoja na kerubi mlinzi na mtiwa mafuta kwenye mlima wa Mungu (Ezekieli 28:14).

Ezekieli 28:14-18  Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. 16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto. 17 Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama. 18 Kwa wingi wa maovu yako, katika uovu wa uchuuzi wako, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao.

 

Hapa tunaona Shetani akiitwa mfalme wa Tiro. Alitupwa duniani. Alikuwa mpeleka nuru au Lusifa, Nyota ya Asubuhi au Nyota ya Siku ya sayari.

Isaya 14:12-15 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.

 

Hapa huyu Mpeleka Nuru, au Nyota ya Asubuhi alijaribu kujiinua juu ya Nyota wengine wote wa Mungu na kutaka awe kama Mungu Aliye Juu Sana. Shetani hakuridhika kule kuwa kwake mmoja kati ya wale Nyota wengine wa Mungu na Mwana wa Mungu akiwa kama kerubi aliyetiwa mafuta afunikaye. Alitaka awe kama Mungu Aliye Juu Sana.

 

Hakuridhika na kuwa kwenye umbo la Mungu, akiwa na umbo na asili ya kimbinguni, Shetani alitaka kujitwalia haiba ya kuwa sawa na Mungu. Kwa sababu hii alitupwa hadi chini duniani. Lakini angali bado anaruhusiwa kweda na kuingia hadi kwenye kiti cha enzi cha Mungu.

Ayubu 1:6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 

 

Wana hawa wa Mungu walikuwa wameyaasi mapenzi na makusudi ya Mungu kwa upande mwingine wa gharika kuu kama tunavyoo kwenye Yoshua 24:14-15.

Yoshua 24:14-15 Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. 15 Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana. 

 

Uasi ulikuwa ni mchakato endelevu kama tunavyoona kwa kushirikiana kwao na malaika hawa waasi.

Mwanzo 6:2-4  wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua. 3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini. 4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.

 

Wana hawa wa Mungu walikuwa ni wale Malaika walioasi. Waliacha makao yao ya kwanza na kufuata tamaa zao mbaya.

Yuda 6-7  Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu. 7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 

 

Kristo hakutaka kuwa na usawa wowote na Mungu, bali aliyatoa maisha yake kwa amri na mapenzi ya Mungu. Tutalielezea vyema jambo hili hapo chini. Alifanya hivyo ili kuwasuluisha na kuwapatanisha Watakatifu akiwa kama Kuhani Mkuu.

 

Melkizedeki alijulikana pia kuwa ni kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana (soma jarida la Melkizedeki (Na. 128)) na Masihi alijulikana pia kuwa ni kuhani milele wa aina ya Melkizedeki (Zaburi 110:4; Waebrania 7:1,11). Bwana huyu ambaye ni Bwana wa Daudi ndiye anayetajwa kwenye Zaburi 110:1 kama ndiye aliyeambiwa aketi mkono wa kuume wa Bwana hadi hapo atakapowaseta chini ya miguu yake maadui wa Bwana wa Daudi (Masihi). Huyu Bwana ambaye ni Masihi waliteuliwa na kuwekwa wakfu na Bwana kuwa ni kama kuhani milele wa aina au mfano wa Melkizedeki. Huyu anayeitwa Bwana hapa, ni Mungu Baba ambaye ni Bwana wa Masihi na ambaye ndiye kwa hakika andiko hili ndiye linayomita Masihi.

 

Kristo au Masihi anajulikana kama Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana kwenye Agano Jipya kwenye Marko 5:7 na Luka 8:28.

 

Masihi alitwaa mwili wa kibinadamu na kuishi ili iwezekane kusulibiwa ili kutolewa dhabihu. Hii ilifanywa tena kwenye utoaji wa dhabihu za hekaluni za Upatanisho wakati kuhani mkuu alipoingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja kwa mwaka na damu ya dhabihu. Masihi alifanya hivyo kama tunavyoona kwenye waraka kwa Waebrania. Upatanisho huu wa dhabihu ya damu ilikuwa ni kwa ajili ya kuwapatanisha Watu na Mungu kwa njia ya mpango asilia wa Mungu ambayo Mungu amewapa Watu wake. Malaika waasi waliikataa njia hii ya kufikiri na kutenda ambayo ndiyo njia ya Mungu. Kristo hakuwa sawa na Mungu lakini, akiwa kama Mwana wa Mungu, alikuwa mtiifu. Hii inaelezewa kwenye Wafilipi 2:6 ambayo ni imepotosha kwenye tafsiri ya KJV. Tafsiri hii ya KJV inalitaja andiko la aya za 5-7 kama:

Wafilipi 2:5-7  Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

 

Andiko linajulikana sasa kukubalika na wanazuoni wasomi kuwa halipo sahihi tafsiri yake. Tafsiri ya RSV inasema hivi:

Wafilipi 2:5-7  Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

 

Maana yake ni kwamba kuwa sawa na Mungu halikuwa jambo la kushikiliwa sana [kama Shetani alivyojaribu kufanya], ambapo kuna maana iliyo kinyume chake kabisa na tafsiri ya KJVNeno linalotamkwa arpagmon hapa lina maana kuwa ni kitendo cha kujitwalia kwa nguvu, ambalo ni uporaji au booty au thamani. Thayer alilisemea hilo kwenye (ukurasa wa 74) na anafafanua maana ya Wafilipi 2:6 kwenye kipengele kijulikanacho kama morphe (ukurasa wa 418). Chembe hii ya hisia ya usawa haikuonekana kama ni kitu cha kushikamananacho au kujivunia sana kabisa.

 

Tafsiri ya the American Standard Version inafanya mrejesho wa tafsiri nyingine ya KJV iliyochapishwa mwaka 1901 ikirudia na kulisahihisha andiko la Wafilipi 2:6 kusahihisha makosa yaliyofanywa kwenye Maandiko ya tafsiri ya Authorised Text. Inasomeka hivi:

ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

 

Tafsiri nyingine ijulikanayo kama The Jewish New Testament [Agano Jipya la Kiyahudi] (tafsiri ya David Stern) inasema kuhusu ayah ii ya 6 hivi:

ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 

 

Wana wa Mungu wote walichukuliwa kuwa ni malaika au wajumbe wanaomwakilisha Mungu Aliye Juu Sana. Hakuna walichokifanya kwa mamlaka au utashi wao wenyewe. Matendo yao yote yalikuwa ni sawasawa na mapenzi ya Mungu (Luka 11:2; Yohana 5:30).

Yohana 5:30  Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.

 

Elohim wa Israeli alikuwa malaika. Alimtokea Ibrahimu na alikuwa ndiye Mngu wa Ibrahimu na ndiye alikuwa Mungu wa Ibrahimu Isaka na Yakobo. Elohim huyu wa Israeli alikuwa pia ni Malaika wa Ukombozi kama anavyotuambia Yakobo.

Mwanzo 32:1 Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye.

 

Wakati huohuo alipokuwa akiwasiliana na malaika hawa, na walikuwa wengi, aliongea na Malaika wa Wokovu akiwa mmoja.

Mwanzo 48:13-16  Yusufu akawaweka wote wawili, Efraimu katika mkono wake wa kuume, kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli; na Manase katika mkono wake wa kushoto, kuelekea mkono wa kuume wa Israeli, akawasogeza karibu naye. 14 Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye aliyezaliwa kwanza. 15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, 16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.

 

Malaika wa Yahovah (Yehovah) anatambuliwa kama Masihi na pia kama Elohim na Mwana wa Mungu (soma jarida la Malaika wa YHVH (Na. 024)). Alikuja kama Mkombozi kwa njia ya kuzaliwa kwake tena duniani. Kwa hiyo yeye sasa ni kicchwa cha wateule ambao ni watu wa nyumbani mwake Daudi chini ya Masihi akiwa kama elohim. Zekaria 12:8 inaonyesha kuwa elohim alikuwa pia Malaika wa Yahovah.

Zekaria 12:8  Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.

 

Malaika wa Bwana anayetajwa hapa ni Yehovah kwenye andiko hili (soma kamusi ya Green’s Interlinear). Neno Mungu kwenye andiko hili ni Elohim. Andiko hili linaonyesha kwamba Elohim aliye kwenye maandiko haya ni Malaika wa Yahovah pia au YHVH na kwamba watu wa nyumbani mwa Daudi (kwa maneno mengine, wateule) watakuwa kama elohim. elohim. Elohim aliye kichwa cha nyumba ya Daudi ni Masihi.

 

Masihi hapa alifanyika kuwa monogenes theos au mzaliwa pekee wa Mungu aliye kwenye Yohana 1:18. Wakati alipokuwa prõtotokos wa Wana wa Mungu, elohim, alipokufa alifanyika kuwa mwana wa pekee aliyezaliwa na hivyo kuwa mzaliwa wa pekee wa Mungu au monogenes theos. Tafsiri ya the Receptus inamuita monogenes uion au mwana mzaliwa wa pekee. Kwa jinsi hiyo, alikuwa ni mwana pekee wa Mungu aliyekuwa anatarajiwa kuzaliwa – kati ya wana wengine wote waliosalia kama roho. Hatujazaliwa tukiwa kama wana bali ni wana tuioasiliwa wa Mungu.

 

Kwa hiyo basi inamaana kuwa kuna elohim mkuu na mdogo. Huyo Elohim mkubwa alijulikana kama Mungu Aliye Juu Sana, au Mungu Mwanyezi (Mwanzo 14:18-20,22). Kumbukubu la Torati 32:8 inaonyesha kwamba Mungu huyu Aliye Juu Sana ndiye aliyeyagawa mataifa. Kama tulivyoona, kwa mujibu wa Maandiko ya kwenye Tafsiri ya the Masoretic Text (MT) ilikuwa ni kwa mujibu kama ilivyo hesabu ya wana wa Israeli. Hata hivyo, tafsiri ya Septuagint (LXX) inasomeka kama sawasawa na idadi ya malaika wa Mungu. Tafsriri ya DSS inaonyesha kwamba maana iliyo kwenye lugha ya Kiebrania yalisema kuwa sawasawa na (wana wa Mungu) miungu (au bene Eliym).Israeli alifanyika kuwa ni sehemu ya Yahova (Yehova). Hii inatupelekea sisi kwenye kutofautisha kati ya hawa Yehova wawili. Biblia imetanabaisha kwa uwazi sana kuwa kuna Yehova wawili. Yehova Mliye Juu Sana na Yehova wa Israeli na viumbe wengine wanaobeba jina na wajihi huu.

 

Ni kama tulivyojionea hapo juu pia, kamusi ya Strong inaonyesha tofauti kati ya Yehova Aliye Juu Sana na Yehova wa Israeli. Tofauti ya kwenye majina ni kwamba Yehovih anatajwa kuwa ni mku na Yahovah anatajwa kuwa ni mdogo anapotumika peke yake. Wakati neno Yahovah linapotumika kwa kumtaja yule mkuu, kwa kawaida linajumuisha na anayestahili kama vile Yahovah wa Majeshi. Idadi sahihi zilizo kwenye kamusi ni zile za SHD 3068 na 3069. Kamusi ya Strong inasema kuhusu Yehovah wa SHD 3068  kwamba lilikuwa ni jina la kitaifa la Kiyahudi au la Wayahudi. Anasema kuwa jina Yehovah a kwenye SHD 3069 linatumika kwa ajili ya Adonai [ambaye ni Bwana Yehovih] na linatamkwa na Wayahudi kama Elohim ili kuzuia kurudiwa rudiwa matamshi hayohayo, kwa kuwa mahali penginepo limetamkwa kama ilivyo kwenye SHD 3068 kama Adonai wa kwenye SHD 136 – huyu akiwa ni Mungu.

 

Hivyo, Wayahudi wanajua kwamba kuna walengwa wawili hapa, mmoja akiwa mkuu na mwingine mdogo. Kama tulivyojionea, Masihi anajulikana kuwa ndiye anayeongelewa kwenye Zaburi 45:6-7 ambaye alikuwa ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu wake.

 

Zekaria 2:3 inaonyesha kwamba Malaika wa Yahovah (ambaye hapa ni wazi sana kuwa ni Masihi) alimpa ujumbe Zekaria kuhusu ujio wake katika Israeli kwa maongozi ya Bwana wa Majeshi. Tofauti inaonekana wazi sana kwamba tunaomungelea Masihi na Mungu Baba ambaye ni Bwana wa Majeshi.

Zekaria 2:8-12 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake. 9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma. 10 Imba, ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa kati yako, asema Bwana. 11 Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwako. 12 Na Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena. 

 

Tofauti iliyopo kati ya Yahovah wa Israeli anayeitwa elohim na eloim wake anayeitwa Eloah au Mungu Mwenyezi. Bwana wa Majeshi, ni tofauti ambayo imepotea kwenye lugha ya Kiingereza ambako kuna jina linguine la Mungu. Nia yake haijaanikizwa bado kwa wasomaji wake.

 

Masihi atawarithi Yuda wakiwa ni sehemu na milki yake katika nyakati za mwisho. Atauchagua tena Yerusalemu atakaporudi mara ya pili. Harakati hizi za Masihi zaweza hatimaye kuparaganyikia mbali kwenye migawangiko kwa mkururu.

 

1.    Tukio la kuzaliwa kwake tena hapa duniani (soma mkururu wa majarida yaliyoorodheshwa kwenye Programu ya Mafundisho ya Biblia (Na. B1)).

 

2.    Mkururu Mwandamamo wa Makanisa (soma jarida la Nguzo za Filadelfia (Na. 283).

 

3.    Nyakati za Mwisho (soma majarida ya Jeshi la Gideoni na Nyakati za Mwisho (Na. 022); Maonyo ya Nyakati za Mwisho (Na. 044)Vita na Mapigano ya Nyakati za Mwisho na Vitasa vya Hasira ya Mungu (Na. 141B); Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na. 192)Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwisho (Na. 219); Mpingakristo Kwenye Teolojia ya Kanisa la Kwanza na Nyakati za Mwisho (Na. 299F).

 

4.    Kurusi kwa Masihi (soma jarida la Kurudi kwa Masihi: Sehemu va I (Na. 210A)).

 

5.    Milenia (sawa pia na jarida la Milenia na Unyakuo (Na. 095)); Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300).

 

6.    Hukumu (soma majarida yaliyoorodheshwa kwenye mkururu wa Programu ya Masomo ya Biblia (Na. B1)).

 

7.    Mji wa Mungu (soma kwenye jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)).

 

Jarida hili linatumika kama utangulizi wa mkururu wa majarida yenye kichwa hiki cha maneno ambayo mengi yake yamehesabiwa na kujumuishwa ndani yake.

q