Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[076B2]

 

 

 

Kristo na Malaika Mkuu Mikaeli

 

(Toleo La 1.0 06072013-06072013)

 

Elohim wa Israeli aliye kwenye maandiko ya Agano la Kale hakujulikana kuwa ni Mungu wa Pekee wa Kweli wala kuchukuliwa kuwa ni huyo kabisa. Bali zaidi tu ni kwamba alichukuliwa kama elohim msaidizi ambaye yeye mwenyewe alikuwa ni elohim ambaye Mungu alikuwa juu yake huyo Eloah. Kiumbe huyu na Mungu wake Eloah wanaonyeshwa kwa wazi kwenye maandiko ya Agano la Kale na Agano Jipya, na kudai vinginevyo ni upotoshaji mkubwa sana na wa makusudi.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ă 2013 Wade Cox)

(tr. 2017)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Kristo na Malaika Mkuu Mikaeli



Kenye makala yake ijulikanayo kama Question and Answer Section, [Makala ya Mwaswali na Majibu]  (Toleo la Julai-Agasti 2013 | Jarida la Tomorrow’s World [Ulimwengu wa Kesho]), Kanisa liitwalo the Living Church of God lilichapisha swali la aina ya Dorothy Dix ambalo lilihusika na masuala nafasi ya Kristo kwenye Agano la Kale. Liliacha kwa kitambo kuficha ukweli wa teolojia yao ya Kiditheism (soma jarida la Uditheism (Na. 76B)); na madai yao kwamba Kristo alikuwa ndiye yule Mungu wa Agano la Kale na kwamba Baba hakudhihishwa kwenye Agano la Kale. Madai haya ni ya uwongo kabisa kama tutakavyoona huko mbele.

 

Mhariri anaanza kwa kuuliza Swali linaloonekana kuwa liliandaliwa ili kupinga habari kwamba kama Kristo anatajwa kwenye Agano la Kale ndipo atakuwa ni Mikaeli akiwa ni kiumbe aliyekuweko akiishi kwenye kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi duniani. Ukweli ni kwamba, jina la Mwana wa Mungu lilipaswa litangazwe kama tunavyoona kutoka kwenye swali lililo kwenye Mithali 30:4 ambapo panasema: Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake? Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake? Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?

 

Jina la Mungu Mmoja wa Kweli limetolewa kwenye aya hiyohiyo inayofuatia ya 5. Kila neno la Mungu limethibitishwa... na neno lililotumika kumtaja Mungu kwenye Kiebrania ni Eloah ambalo ni la umoja na inakubali kutokuwa na uwingi kwa namna yoyote ile. Jina la Mwana yapasa liwekwe au liingizwe pahala pengine. Tunaweza sasa kulitafakari jibu lao kwenye swali hili. 


Je, unapajua mahala unapoweza kumkuta Yesu Kristo kwenye Agano la Kale?

 
Swali:
Mchungaji wa rafiki yangu anasema kuwa malaika mkuu Mikaeli ni roho yuleyule mwenye mwonekano wa kimwili kama alivyokuwa Yesu Kristo. Biblia inasemaje hasa kuhusu ujulikano wa Mikaeli na Kristo?
 
Jibu: Madhehebu yanadai kimakoa au kwa upotoshaji mkubwa kwamba Yuda 1:9 inamrejekea au kumtaja Yesu Kristo pamoja na rejea au kumtaja “Malaika Mkuu” anayejulikana kama Mikaeli. Mawazo yao ni kwamba neno hilo ambalo kwa Kiyunani huandikwa archaggelos kwa maana ya “malaika mkuu,” ni la umoja, kwa hiyo ni lazima liwe linarejelea au kutaja uwepo wa malaika mmoja aliye mkuu na mwenye mamlaka makubwa ya aina zake. Na ndipo wanapoihusisha aya hii na ile ya 1 Wathesalonike 4:16—kuna moja tu nyingine ya kwenye Agano Jipya hutumia neno hili archaggelos—ambayo inasema, "Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu." Mawazo na nadharia hii ni ya makosa na upotoshaji, kwamba je, kurudi kwa Kristo kwa hiyo ni lazima kuambatane na roho hiyohiyo ya mwonekano wa kimwili kama ya malaika Mkuu Mikaeli.

 

Ni kweli, kumuelezea malaika mkuu kama anayeshuka kutoka juu au mbinguni “akiwa na sauti ya malaika mkuu” kunafanya iwe ni kama inaeleweka au kukubalika kama kumwelezea mtu mwanaume akiimba “pamoja na sauti ya mwanaume.” Kwa namna nyingine, kama mwimbaji alikuwa na nguvu nyingi sana kuliko sauti nyingine inayojulikana, zaidi ya uezo wa kibinadamu, lingekuwa ni jambo la kiasilia kulinganisha nguvu zake na kwa sauti kubwa zaidi ijulikanayo. Hivi ndivyo sasa tunavyoweza kuyaelewa vizuri zaidi maneno ya Mtume Paulo yaliyo kwenye 1 Wathesalonike 4:16.
 
Ni Malaika wake? Hoja zingine zilizopangiliwa kimakosa au kiupotoshaji zinadhaniwa kuwa iwapo kama Ufunuo 12:7 inamwelezea Mikaeli na jeshi la “malaika wake” wakipigana na Shetani (Joka), basi ni lazima Mikaeli awe ni kiongozi wa jeshi hilo, na ni lazima atakuwa na haiba sawa nay a Yesu Kristo, ambaye Maandiko Matakatifu mahali pengine yanamwelezea kama ni kamanda wa malaika wenye nguvu nyingi.


Hii, pia, ni dhana na nadharia potofu. Kila jeshi lina madaraja ya vyeo na ngazi mbalimbali, kama vile sajenti na jenerali ambao wote wawili wanaweza kuliita kundi la maaskari “watu wangu.” Mikaeli naye akiwa na “malaika wake” hakumjumuishi tena Mikaeli kutoka kuwa ni mmoja wa malaika aliye chini ya Yesu Kristo! Jaribu kufikiria, pia, maana ya vita ya Mikaeli. Maandiko Matakatifu yanamwelezea Mikaeli kama anayepigana na joka na malaika zake! Ndiyo, Shetani ana “malaika zake” na siye Yesu Kristo! Na ni vivyohivyo alivyo Mikaeli! Shetani alishagawahi kuwa mfalme wa malaika wote—wakati alipokuwa mkamilifu katika njia zake zote (Ezekieli 28:14–16)! Kuwepo kwake akiwa kama Lusifa mleta nuru au mwenye mng’aro, Nyota ya Mchana (nyota likiwa ni jina lingine la malaika na mjumbe kwa Kiebrania), akimweka yeye sio mahala pengine popote bali pa chini zaidi kuliko kuwa ni malaika mkuu mwenye nguvu au “kerubi afunikaye.”

 

Maandiko Matakatifu yameweka wazi kwamba hakuna malaika aliye zaidi ya kuwa mtumishi. Malaika hawapasi kuabudiwa wala kuombwa (Wakolosai 2:18, Ufunuo 22:8–9), na wana kikomo cha kiuweza. Wote wawili, yaani Mikaeli na Kristo walikuwa viumbe, na kama tungali waona tusingeiona tofauti kubwa sana kati yao na hata kwa jinsi walivyoshughulika na Shetani. Kumbuka kwamba Mikaeli alikataa kumkemea Shetani kwenye waraka wa Yuda 1:9—ni tafauti na ilivyokuwa kwa makemeo makubwa aliyoyafanya Yesu Kristo akimkemea kama tunavyoona kwenye Luka 4:8! Kumbuka pia kwamba Yuda anamtaja Yesu Kristo moja kwa mojakwenye Yuda 1:1 na Yuda 1:17. Kwa namna nyingine anaunganisha na aya yake ya 9 inayomwelezea au kumtaja Mikaeli pamoja na rejea nyingine yeyote inayomtaja Yesu Kristo. Anawachukulia wao kuwa ni kama viumbe wawili tofauti—ambao ni pamoja na walivyo wao!

 

Ule Mwamba Ulikuwa ni Kristo! Kwa hiyo basi, hivi alikuwa wapi Yesu Kristo kabla hajaja hapa duniani? Maandiko Matakatifu yanaeleza kwamba Neno—Logos—alikuwa Mungu, na alikuwa pamoja na Mungu Baba tangu milele yote (Yohana 1:1). Huyu Neno hakuwa ni malaika aliyeumbwa. Kwa kweli, alikuwa ni Neno—na siyo Mungu Baba—ambaye Waisraeli wa hapo zamani waliyefuatananaye (1 Wakorintho 10:4). Yesu Kristo aliwaambia Waisraeli kinagaubaga kabisa kwamba hawakumjua bado Mungu Baba—bali ni Kristo tu ndiye aliyemjua yeye—na ilikuwa ni Yesu Kristo ambaye ndiye angemdhihirisha Baba kwao (Yohana 1:18; 17:25)! Hakuna malaika wa kawaida angefaa kukubalika sadaka yake kwa ajili ya wenye dhambi; bali ni Mwana wa pekee wa milele wa Mungu tu, ndiye angefaa na kustahili kulijaza pengo hilo. Mtoto au Mwana huyo ni Yesu Kristo. Maandiko Matakatifu yanaeleza na kudhihirisha wazi sana kwamba Mikaeli malaika mkuu ni kiumbe aliyeumbwa ambaye anatumika na kuhudumu chini ya Kristo.”

Michanganuo hii inaangukia kwa kuhusiana na ukweli wa kwamba Kristo anatajwa rasmi kabisa kuwa ni kama nyota ile itakayokuja kutoka kwa Yakobo (Hesabu 24:17) ambaye ndiye Israeli na Yuda kwenye unabii ulio kwenye Torati. Hata hivyo, wakati kunapokuwa na hawa “wanazuoni” waoga.

 

Rejea iliyo kenye Yohana 1:18 inaangukia kushughulikia ukweli wa kwamba Kristo alikuwa ni monogenes theos ambayo maana yake ni ni theos mzaliwa wa pekee au mwenye mamlaka ya Mungu na aliye kifuani mwa baba na alitangazwa au kunena. Kwa hiyo alikuwa ni malak au mjumbe (soma jarida la Kwenye Maneno: Monogenes Theos Kwenye Maandiko Matakatifu na Mapokeo (Na. B4)). Haikuwa ni muda kitambo sana uliopita kwamba watu hawahawa walikuwa wanalitumia andiko hili ili kueneza mafundisho ya Utatu na kukataa umuhimu wake na maana yake.

 

Kumbuka kwamba imeonyeshwa vizuri sana kwamba Kristo alikuwa ni kiumbe aliyekuwa pamoja nao jangwani na ilikuwa ni yeye aliyeonekana kuwa ni malaika wa uwepo wake ambaye ndiye aliyemkabidhi torati Musa pale Sinai. Wanalazimishwa kuukubali ikweli huu. Uwepo wa Yesu Kristo katika kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi duniani imeelezewa kwa kina kwenye jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243).

 

Kumbuka pia kwamba kuna maandiko mengi sana yaliyoachwa nje ya mfano huu yanayoonekana kuyakanganya Maandiko Matakatifu na kuendeleza mafundisho ya kizushi ya Kiditheist na madai ya uwongo na mapotofu kwamba Mungu Baba hakuwa anajulikana tangu kwenye Agano la Kale.

 

Kumekua kila mara ikifundishwa kwenye imani za Kisabato kwamba Kristo aliitwa mahali penginepopote kwenye Agano la Kale kuliko jina lile basi atakuwa Mikaeli. Hayo ndiyo yalikuwa ndiyo mafundisho ya imani ya SDA hadi pale ilipojitangaza kuwa imegeukia rasmi imani ya Utatu au Utrinitarian mwaka 1978.  Lilikuwa ni fundisho muhimu na linaloainisha imani yao kwao, pamoja na yalivyokuwa Makanisa lingine linalojulikana kama Kanisa la Mungu la Siku ya Saba maarufu kama Churches of God (Seventh Day) ambako ndiko walikoyachukua mafundisho haya, kwamba Malaika Mkuu wa Agano la Kale alikwa ni Mikaeli, na kwamba kiumbe huyo alikuwa ni Kristo. Kanisa la WCG, na machipukizi yake (isipokuwa kwa baadhi yake tu) ndiyo hayakuyaendeleza mafundisho haya hata kwa pale walipoanzisha na kuingiza teolojia potofu kutoka kwenye Uditheism “Mafundisho Mapotofu ya Yakizushi ya Nguvu Mbili za Kiuungu” ambayo baadae ilichukuliwa na kuingizwa kwenye Ukristo yaliyotafuta kudai kwamba kulikuwa na viumbe wawili walio miungu wenye haiba sawa kwa umilele na kwa kila kitu na ambao walikuwepo kabla ya uumbaji na mmoja wao aliaamua na kuhiyari kuja hapa duniani na kuwa ni mwana wa mwingine. Haya siyo mafundisho ya kukubalika kwenye imani ya Kikristo bali yalichukuliwa kutoka kwenye teolojia ya Kibinitarian ya dini potofu za waabudu mungu Jua Attis wa Roma na Adonis na Orisis wa pande za Mashariki mwa Mediterranean na kutoka kwa Mithras na Baali kwenye dini nyingine potofu ya waabudu jua wa huko Asia Ndogo. Mwenzi wake alikuwa ni mungumke mama aliyejulikana kama Easter au Ishtar au Cybele au Isis au Ashtarothi mwenzi wa Baali. Mafundisho haya yalichukuliwa kutoka kwa waabudu Baali na yalilaaniwa na kukatazwa kwa nguvu zote kwenye Biblia.

 

Kanisa la LCG na makanisa mengine yaliyochipuka pamoja nalo yamekuwa yakiyapuuza kwa makusudi kabisa maandiko mwongozo ya Biblia yanayoonyesha kwa wazi sana kwamba malaika wote ni wana wa Mungu na kwamba Shetani naye ni mwana wa Mungu. Ayubu 1:6 na 2:1 zinaaonyesha kwamba wote hao walikuwa wanaruhusiwa kwenda kwenye kiti cha enzi cha Mungu pamoja na Shetani na alikuwa na fursa kama hiyo ya kutembelea katika kipindi cha Ayubu ambaye alikuwa ni mkazi wa eneo la Isakari katika Mashatiki ya Kati (huenda ni huko Midiani). Wana hawa wa Mungu walikuwa elohim ambao walikuwa ni jeshi kubwa la malaika na walijulikana kama hivyo na wanazuoni au wasomi wa Biblia kama vile Bullinger na wengineo. Wana wa Mungu waliitwa elohim ambalo ni neno la umoja linalommaanisha Mungu kama ni kiumbe mwenezi. Elohim ametajwa kwenye Ayubu 2:1 lakini jina Eloah limetumika mara nyingi likimtaja na kumaanisha Mungu wa Pekee na wa Kweli kwenye kitabu chote cha Ayubu. Ayubu 1:6 inamtaja Shetani kuwa ni miongoni mwa wana wa Mungu. Kwa hiyo anatumika kumjaribu Ayubu na kumtesa. Ayubu 2:1 pia anamwonekano huohuo wakati wana wa Mungu walipojihudhurisha mbele za Mungu na Shetani alikuwa pamoja nao miongoni mwao. Kwa hiyo hakuna mashaka babisa kwamba kulikuwa na wana wengi wa Mungu katika nyakati za Agano la Kale na Shetani alikuwa ni miongoni mwao na wote waliruhusiwa kujongea kwenye kiti cha enzi. Wana hawa wa Mungu waligawanyika kwenye vyeo au madaraja na tunaona kwenye Ayubu 38:4-7 kwamba Mungu Mmoja wa Kweli aliiumba dunia hapo mwanzoni na kwamba wana wa Mungu walijihudhurisha mbele za Mungu muumbaji na Nyota wote wa Asubuhi waliimba kwa furaha wakati walipooonyeshwa uumbaji. Kwa sasa, huyu Nyota wa Asubuhi ndiye mtawala wa ulimwenhu na anatajwa na kujulikana kama  mpeleka nuru au “Lusifa” na hawa viongozi wa Jeshi la Malaika wa Mbinguni walikuwa ni watawala wa Baraza la Mbinguni ambalo tulionyeshwa pale Sinai waliwa wameanzishwa tena kwenye Maskani kama baraza lililojulikana kama Sanhedrin la watu au wajumbe Sabini jumlisha Wawili, na ambaye waligawanyika kwenye Baraza la Mbinguni la kwenye Ufunuo sura za 4 na 5 la Makerubi Wanne na lenye Wazee Ishirini na nne na Mwana Kondoo wa Mungu. Baraza la nje lilikuwa na wazee wengine ishirini na wawili wakifanya jumla ya wanabaraza 72. Hili ndilo lilikuwa baraza la Sanhedrin pia la kutoka Sinai na la wanabaraza Sabini na wawili au Hebdomekonta [Duo] lililoanzishwa na Kristo na wazee wa kanisa (Luka 10:1,17).

 

Sasa wana wengi wa Mungu walitumwa kwa wanadamu kama wajumbe na kwamba neno lenyewe lilikuwa Malak kwa Kiebrania na kwa Kiyunani aliitwa Aggellos. Neno hilo lilimaanisha tu mjumbe na elohim walikuwa wote wana wa Mungu kama elohim hadi walipotumwa kwa wanadamu wakiwa kama malak. Na ndiyo sababu wote waliitwa kama Yahova na jeshi la kibinadamu walionyeshwa mbele zao (Gr. proskuneo). Neno hilohilo limetumika kwa wateule wakati wale wanaosema kuwa wao ni Wayahudi bali siyo lakini wakituama kwenye proskuneo mbele za wateule wa Kanisa la Wafiladelfia kwenye Ufunuo 3. Waumini wa imani ya Kibinitarian waliomuabudu mungu Attis huko Roma walileta mafundisho yao potofu ya kizushi na kuyaindiza kwenye Ukristo tangu mwaka 175 BK. Ili kuiingiza kwa imani ya Kibinitarian ya mungu Attis iliwalazimu kumuinua juu na kumtukuza Kristo kwenye kiwango cha juu na kumfanya aonekane yuko juu zaidi kuliko wana wengine wote wa Mungu au elohim. Walilifanya hilo kwa kuunda daraja na kuwaita wao kuwa “Malaika” kutokana na neno aggellos au mjumbe ambayo ilikuwa ni tafsiri ya neno malak au mjumbe kwenye Agano la Kale. Na kwa hiyo waliwafanya watofautiane na Kristo na wakalitumia neno elohim au theos wa yeye na Baba peke yake. Wakiwa wamefanya upotoshaji huu ndipo walimjumuisha Roho Mtakatifu kuwa ni kama wa tatu kwenye mjumuiko huu wa Mungu wa Utatu mwaka 381 BK kwenye Mtaguso wa Constantinople na kuthibitisha au kuupa nguvu kwenye Mtaguso wa Kalkedon mwaka 451. Mchakato wenyewe na teolojia yake vimeainishwa kwa kina kwenye jarida la Upotoshaji wa Wabinitarian na Watrinitarian Kuhusu Teolojia ya Mwanzon ya Uungu (Na. 127B).

 

Tunajua kwamba Jeshi la Malaika wa Mbinguni liligawanyika kwa makundi 72, kama mataifa yalivyoorodheshwa kati ya zama za kale na kuwa sabini na mbili na waligawanyika sawasawa na idadi ya wana wa Mungu. Hii imeandikwa au kuorodheshwa kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8 (soma tafsiri za RSV na the DSS na the LXX ambamo neno elohim limetafsiriwa kuwa Aggellou Theou), na andiko lililo kwenye Sura ya 32 lilimwonyeshwa Eloah kuwa ni Mungu linashangaza sana. Ni andiko hili ndilo linamwonyesha elohim kuwa ndiye anayewapatia milki Israeli wakiwa ni urithi wake ambaye pia anatajwa kama Yahovah wa Israeli. Huyu ndiye elohim ambaye alishinana kwa mweleka na mababu wa imani na aliyenena na Ibrahimu na Hajiri. Andiko la Kumbukumbu la Torati 32:8 liligeuzwa maana na kupotoshwa na baraza la Sopherim ili kuepuka ukweli wa kwamba Yahovah aliyewamilikisha nchi Israeli alikuwa ni elohim mdogo aliyetajwa na kumaanishwa kwenye Zaburi 45:6-7 na ameelezwa au kuoneshwa kwenye Waebrania 1:8-9 kuwa ni Yesu Kristo. Upotoshaji huu wa kugeuza maana halisi iliyokusudiwa ulifanyika mara 134 kwenye Agano la Kale na jopo la Sopherim. Zaburi inalitaja pia baraza la elohim na Zaburi 82:6 inasema kuwa wao wote ni Miungu. Kristo anajitaja mwenyewe kama mmoja wa elohim hawa kwenye Yohana 10:34-36 na ndiyo sababu iliyowaghadhibisha hata wakamuua na walipotosha maana ya andiko la Agano la Kale ili kuficha ukweli huo. Andiko lililo kwenye Danieli linamuonyesha wazi kabisa Mikaeli kuwa ni kama Mfalme Mkuu asimamaye kwa niaba ya taifa la Israeli na kwamba kwa kuwa Kristo ni Mwana wa Mungu aliyetajwa kwenye Agano la Kale, ambaye Mungu anampinga mtu yeyote anayedai kuijua sana Biblia na kutangaza, jina lake ni Mikaeli kama tunavyoona kwenye Danieli 12:1 na penginepo. Hivi ni vita vya Nyakati za Mwisho wakati atakapotumwa aje kuwakomboa Israeli. Hii Zekaria 2:8-13 ambako Yahova wa Majeshi, Mungu Mmoja wa Kweli, Elyon, anapomtuma Yahova wa Israeli huko Yerusalemu na kwa mataifa yaliyowapotosha, kwa kuwa yeye augusaye Yerusalemu anaigusa mboni ya jicho lake [inasomeka jicho langu]. Huyu Mungu Mmoja wa Kweli aliyetajwa kwenye Agano la Kale kama Eloah, na pia kwa mwandiko wa Kikaldayo Elahh. Yeye ndiye anayestahili kuabudiwa na kutolewa dhabihu za Hekaluni na ndiye ambaye torati na sharia zinatoka kwake (Ezra 4:23-7:26). Neno Yahova ni la nafsi ya tatu ya vebu yenye maana ya “anasababisha iwe” linalotokana na Kutoka 3:14 ‘eyeh ‘asher ‘eyeh maana yake ni Nitakuwa kama Nitakavyokuwa (soma pia tafsiri  ya Annotated Oxford RSV). Kwa hiyo Eloah alifanyika Ha Elohim au Mungu kama kichwa au kiongozi wa kiumbe jumuishi.

 

Tunawezaje kujua kwa hakika kwamba elohim ambaye alikuwa Mungu wa haraka wa Yakobo alikuwa malak au aggellos (LXX) aliyemkomboa yeye, na mababa wengine wa imani kama Ayubu. Ni kwa sababu tu tunaambiwa kwamba ilikua ndiyo ilivyokuwa kwa Yakobo na pia kwa Ayubu na kwa Musa, aliyeandika vitabu vyote viwili, cha Ayubu na cha Mwanzo. Kwenye Mwanzo 48:15-16 tunasoma habari ya Yakobo akiwabariki Efraimu na Manase na ndiye Yusufu akisema:

15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, 16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.  

 

Bilashaka kwamba elohim huyu alikuwa ni malak au aggellos (LXX) kama ni ombi kwa kiumbe mmoja anayebariki barobaro na siyo viumbe. Huyu malak au mjumbe alikuwa ni elohim akiwa kama mmoja wa wana wa Mungu. Tunaona pia kwamba yeye ni kichwa au kiongozi wa watu wa nyumbni mwa Daudi na Israeli kwenye Zekaria 12:8 na wote wakafanyika kuwa elohim. Ayubu anasema pia kwamba mwokozi wake alikuwa ni mmoja wa watu wakuu wa elohim ambao wanafikisha idadi ya viumbe 1000 (Ayubu 33:23-24).

 

Elohim wa Israeli aliye kwenye Zaburi 45 pia alikuwa elohim wake juu yake ambaye alikuwa ni Mungu Mmoja wa Kweli na kiumbe huyo alimuinua na kumtukuza yeye zaidi ya nafasi waliyonayo ndugu zake wote ambao nao walikuwa washiriki kwenye baraza la elohim wa kwenye Zaburi. Huyu elohim mdogo alikuwa ni Kristo (Waebrania 1:1-9).

 

Kwa hiyo haiwezekani kabisa kwa maandiko ya Agano la Kale kudaiwa kuwa hayamtaji wala kummaanisha Mungu Mmoja wa Kweli na kuonyesha kwamba mmoja wa wana wa Mungu ni Yahova mdogo wa Israeli na ndiye inayomjata Biblia kuwa ni Yesu Kristo. Kwahiyo imethibitika kwamba huduma ya lililokua kanisa la WCG na kamanisa mengine yaliyoparaganyika kutoka humo hayajui tu wanachokisema. Wanahubiri mafundisho ya uongo na mafundisho ya miungu ya uwongo na kwa ukweli huo ndiyo maana hawakuachiliwa pia washike na kuifuata Kalenda Takatifu kabisa. Na wala hata Herbert Armstrong hakuachiwa afanye hivyo, aliyewafundisha wao mafundisho haya ya uwongo na mapotofu, bali yeye pamoja na wao hawakuelewa kikamilifu kilichokuwa cha kweli na kwa hiyo ndipo walishimdwa kufundisha vizuri na kiusahihi. 

 

Majina ya Kristo

Kwa kuongezea majina ya Elohim wa Agano la Kale ndipo pia tuna majina mengine aliyoitwa Kristo kwenye Agano Jipya. Injili inamuita yeye kuwa Immanueli ambaye maana yake ni “Mungu pamoja nasi” na wala hakuitwa hivyo kabisa licha ya kuelekezwa na malaika. Aliitwa Yahoshuah aur Joshua kwa Kiingereza (Yoshua kwa Kiswahili) au “Yahovah anaokoa” (au wokovu wa Yaho[vah]) ambalo lilikuwa ni jina la mwanadamu aliyenena na jemadari wa jeshi la Bwana huko Yeriko, aliyeitwa Yoshua mwana wa Nuni, maana yake ni “Wokovu wa Yahova huka kwa njia ya uvumilivu.” Majina mengine ya kinabii ya kwenye Agano la Kale yanapatikana kwenye jarida la Isaya 9:6 (Na. 224). Majina mbalimbali yanayomhusu Masihi kwenye maagano yote mawili yaani kwenye Agano la Kale na kwenye Agano Jipya yanaonyesha kwamba kuna mabadiliko kwenye daraja lake la kicheo kwa namba zote mbili, elohim na malak au aggellos/aggellos mkuu na kama Mwana wa Adamu na majina yenyewe yanabeba maana kama hiyo.

 

Andiko la kwenye waraka wa Yuda linaonyesha wazi Kristo na imani waliyopewa watakatifu mara moja tu kuwa ni kama msisitizo au kiini kikubwa cha andiko lenyewe na andiko la Mikaeli na Shetani linaonyesha kwamba alikuwa ni Mikaeli aliyewaongoza mle jangwani huko Yordani mkabala na Yeriko aliyepigana na Shetabi akiugombea mwili wa Musa na alikuwa ni Mikaeli huyu ndiye aliyekutana na Yoshua huko Gilgali akiwa kama jemadari wa majeshi ya Bwana (soma pia jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)). Huyu ni mfalme mkuu anayesimama kwa niaba ya watu wa Israeli na kama Kristo ametajwa kwenye maandiko ya Agano la Kale kama yanavyosema maandiko ya kitabu cha Mithali kwamba alikuwa ni Mikaeli. Yeye ni malaika mkuu wa Jeshi la Mbinguni akiwa mkuu kwenye komandi na cheo cha Malaika. Soma pia kwenye jarida la Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu (Na. 134).

 

Makanisa ya LCG na UCG na mengine yanayomwabudu Armstrong na kushikilia itikadi zake hayawezi kumudu kukubali kwamba Armstrong alikosea ni kama kwakweli ilivyo vita kwa kujilimbilikizia au kujipatia fedha tu kwa sasa na siyo kwa ajili ya ukweli. Wangeweza hatimaye kukubalia makosa ya kimafundisho kuhusu Tabia na Asili ya Mungu na kisha kuhusu Kalenda.

 

Wao wawajui vya kutosha. Wengi wao hata ni bado Waprotestanti ambao hawajaongoka; ambao hukumu imekuwa ikitolewa na Armstrong kwa Waprotestanti hao ambao haakuwa wanaelewa vizuri Asili ya Mungu kama ilivyoelezewa kwenye maandiko kadhaa wa kadhaa ya Biblia.

 

q