Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[071]

 

 

 

Malaika na Sadaka ya Ibrahimu

(Toleo La 2.0 19941008-19991213)

 

Sadaka iliyotakiwa kutolewa na Ibrahimu ya mwanae Isaka inaelezewa kwa kina mtazamo unaotaka kulifafanua jukumu la Malaika wa YHVH (Yahova) kwenye tukio hili na ambalo halichanganyiki na uweza wa Mungu wa kujua kila jambo. Jukumu la Malaika katika kumponya Ibrahimu linaonekana pia katika kumponya Isaka.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1994, 1999 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Malaika na Sadaka ya Ibrahimu


 


Ibrahimu na Malaika

Biblia inaendelea kumdhihirisha Mungu kwa kupitia Malaika au mjumbe kwa msingi endelevu na wenye utaratibu maridhawa. Mwanzo 16:7 inaelezwa kuwa ni kama inayomuonyesha Malaika huyu.

 

Hadhithi kuhusu jinsi Hajiri alivyomkimbia Sarai (Mwanzo 16:7-13). Malaika anaahidi kwamba atambariki na kuuzidisha mzao wake aitwaye Ishimaeli na ambao ni taifa la Kiarabu. Na kwamba Baraka za watu wa jamii ya Kiarabu inatokana na ahadi hii ya Malaika aliyomahidi Hajiri. Kwenye aya ya 13 Hajiri anamtaja kiumbe aa mtu aliyeorodheshwa hapa kwenye uaya hii kuwa ni kama YHVH, kama Wewe-Ni-Mungu-Unayeona akitumia tu umbo la Mungu, El.

 

Tafsiri ijulikanayo kama Kijani (ya The Interlinear Bible) inaonyesha andiko hili kama hivi:

Malaika wa Bwana akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.  Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai. Malaika wa Bwana akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake. Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi. Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako. Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote. Akaliita jina la Bwana aliyesema naye, Wewe U Mungu uonaye, kwani alisema, Hata hapa nimemwona yeye anionaye?

 

Kiumbe huyu alikuwa hatofautiani na Yule aliyetajwa kama Malaika wa Yahova (YHVH) na pia kama pia Yahova, Yule aliyesemanaye akimuahidi kuongezeka kwake. Ahadi alizopewa Ishimaeli zina maana yake kubwa sana pia. Wazo la kwamba Ishimaeli aliishi kobla ya ndugu zake wote lina maana nyingi zaidi yanayoonyesha matukio ya siku za mwisho.

 

Kiumbe huyu aliitwa kama Yahova tena anamtokea Ibrahimu (Sura ya 17) miaka kadhaa iliyofuatia baadae. Ibrahimu aliongea naye uso kwa uso. Kwenye injili ya Yohana 1:18 kiumbe huyu, kwa hiyo asingeweza kuwa Mungu Baba anayetajwa kwenye malalamioko yake kama ton Theonin kwa Kiyunani) au Eloa. Ananena kama Elohim Shadday (SHD 7706) au Mungu Mwenyezi (mwenye uweza mwingi). Kiumbe huyu alikuwa ni Elohim na tena kwenye uelewa wa maandiko haya hakuwa ni huyu Eloah au Mungu Baba. (Eloah ni jina linaloonyesha Mungu mmoja, kama Allah). Hii inamuweka kiumbe huyu kana Yule aliyetajwa kwenye Zaburi 45:7. Elohim wa Israeli ambaye alitiwa mafuta kuwa Elohim na Elohim (Eloheik) wake ambaye ni Eloah. Kiumbe huyu anaweka agano lake na Ibrahimu na kufanya agano tena na kuubariki uzao wake, yaano wote wawili, Ishimaeli na Isaka. Anafanya agano na uzao wa Isaka milele. Huyu Elohim anatenda mambo yake mjumbe au Malaika wa Yahova, Aliye Juu Sana na ni yeye Mwenyewe ndiye aliyetajwa kama Yahova na pia ni Malaika wa Yahova. Kwenye Mwanzo 18, Yahova anamtokea tena Ibrahimu ... wakati huu akiwa na kundi la watu watatu. Kwenye Mwanzo 18:3 anaelezewa kuwa ni Yahova. Hii ni ya kwanza kati ya jumla 134 ya maeneo yaliyopotoshwa ambapo badala ya kuandika neno Yahova iliandikwa Adonai kwenye tafsiri ya Sopherim (mfuatano wa mambo). (Orodha rasmi ya hizi mara 134 imetolewa kwenye tafsiri ya Massorah, kurasa za 107-115, Toleo la Ginsburg) na imerudiwa kwenye tafsiri nyingine ya The Companion Bible, sehemu ya Nyongeza namba 32. Orodha inamaana. Uingizaji yaliyowahusu Mababa yapo kwenye Mwanzo 18:3,27,30,32; 19:18; 20:4; Kutoka 4:10,13; 5:22, 15:17; 34:9; Hesabu 14:7. Elohim alichukuliwa kwa namna moja na kwa hiyo orodha inahitaji nyongeza.

 

Watu hawa watatu wanaaonekana hapa walijulikana kuwa ni Yahova bila kuwatofautisha. Kwa hiyo wajumbe wengi au malaika (Malak) ndiyo kwayo, majina ya kikazi ya wafalme wa Israeli yalitokana, yalichukuliwa kutokana na jina hili.

 

Ibrahimu alishirikishwa na Yahova kuhusu kuuachilia mji wa Sodoma kama ungekutwa unamcha na kuwa mtakatifu. Viumbe wawili kwenye Mwanzo 19 waliokuja Sodoma (kama alivyoambiwa Ibrahimu) walijulikana kama Malaika. Watu hawa wawili walijulikana kama Yahova, wote wawili walikuwa wamoja na pasipo kutofautia, ambao huenda ndiyo sababu ya Serafi kubadilishwa jina lake kwenye Mwanzo 18. Maangamizo ya Sodoma yalifanywa na Elohim (Mwanzo 19:29). Kwa hiyo tunaweza kuonyesha kwamba jina Yahova au YHVH linendana na mlolongo wa kidaraja la cheo, hadi kufikia kwenye Yahova Aliye Juu Sana, au Eloa, hadi kwa Elohim wa Israeli ambaye ni mdogo na msaidizi wa Mungu, hadi kwa malaika wawili ambao kwa namna nyingine walikuwa ni wasaidizi wake Elohim. Kwa hiyo jina ni la yule mwenye mamlaka aliyopewa na Eloa. Kwa kuhitimisha zaidi ni kwamba tuna viumbe maalumu wanne, ambao wanajulikana kama Mungu kwenye maelezo ya bilbia. Ni wepi hao? Je, wanafanya nini na wanaelekea kufanya nini ili kumaanisha majina yao? Jibu ni kwamba, Kristo ndiye aliyekuwa akiwatokea Israeli na kuanzisha utaratibu wake au imani kwa kupitia Mababa zao watakatifu. Matendo haya hukusu Ibrahimu, Isaka na Yakobo yana maana sana.

 

Kwenye Mwanzo 20:4, kiumbe anayetajwa kama Elohim na Abimeleki, mfalme wa  Gera, alikuja kwake kwa njia ya ndoto alimuamuru amrudishe Sara, mke wa Ibrahimu ambaye alikuwa amemchukua akidhani kuwa ni dada yake Ibrahimu. Kimsingi huyu Elohim ndiye aliyelifanya agano na Ibrahimu na uzao wake. Kwahiyo, wakati Hajiri alipofukuzwa, kiumbe huyu alimlinda kwa ajili ya ahadi iliyotolewa kwa Ishimaeli. Kwenye Mwanzo 21:17-20 tunaona mahali pa ajabu kwamba Elohimu alisikia sauti ya Ishimaeli, ila alikuwa ni huyu Malaika wa Mungu (Elohim) aliyenena na Hajiri. Lakini jambo la ajabu zaidi kuhusu kiumbe huyu, ambaye alikuwa ni Malaika wa Elohim, alikuwa ndiye yeye mwenyewe alikuwa kama Elohim wakati alipomfungua macho Hajiri. Kwahiyo, Elohim aliyerudia ahadi zake kwa Hajiri kwamba alifanya Ibrahimu kuhusu Ishimaeli, kuwa awe mdogo kama Malaika wa Elohim ila pia alitajwa kwake kama Elohim kwa haki yake mwenyewe.

 

Malaika na sadaka ya Isaka

Malaika wa YHVH ndiye kiumbe kile kilichomkataza na kushughulika na Ibrahimu. Malaika alimjaribu Ibrahimu kwa kumtaka atoe sadaka ya mwanae Isaka. Uweza wa Mungu wa kujua mambo yote ulikuwepo bila shaka kama ilivyokuwa sio Eloah aliyehusishwa moja kwa moja.

 

Mwanzo 22:11-12 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee. (Tafsiri ya The Interlinear Bible).

 

Kiumbe huyu hapa anayemjaribu Ibrahimu alitajwa kwa namna mbalimbali kama YahovaElohim na Malaika wa Yahovah. Malaika, ambaye kwa wazi kabisa ni msaidizi hana uweza wa kujua kila kitu. Anaweza kuwa alimjaribu Ibrahimu kwa malengo ya kumuonyesha Ibrahimu na Isaka, akiwa anajua kitakachotokea. Ushahidi wa kibiblia ni kwamba kiumbe huyu amepewa uwezo sawasawa wa kujua kila kitu hapa duniani. Mungu anajua kila jambo na Mungu huyu aonaye majira na au anayefanya hukumu (RSV).

 

Ayubu 24:1 Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?

 

Ayubu 24:1  Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?

 

Dhana au wazo ni la kweli kwamba yeye ndiye ajuaye kila jambo. Tafsiri ya The Interlinear Bible inatoa mwanga zaidi kwenye somo lenye tafsiri ya moja kwa moja zaidi.

 

Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?

 

Andiko hili limechukuliwa kutoka kwenye usemi wa moja kwa moja kwamba Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake? Nusu ya mwisho ni swali linalodai, kwa nguvu, kwamba ni         muhimu kumjua Mungu ili kusiona siku zake.

 

Nusu ya kwanza ina ushauri kwamba wakati sio kipindi kinachotoa dhana kwa Mungu kwa ile ambayo kwayo haijahifadhiwa na yu tayari kufikiwa katika siku zijazo. Ayubu 28:10,24 inaonyesha uweza wa muda mfupi wa kujua kila jambo wa kupewa na Mungu

 

Ayubu 28:10 Hukata mifereji kati ya majabali; Na jicho lake huona kila kito cha thamani

 

Ayubu 28:24 Maana anatazama hata miisho ya nchi, Na kuona chini ya mbingu nzima.

 

Mungu yu kwenye utamalaki kamili wa harakati zote duniani. Uelewa wake wa harakati za mwanadamu ni kamili.

 

Ayubu 31:4 Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?

 

Ayubu 34:21-25 Kwani macho yake ya juu ya njia za mtu, Naye huiona miendo yake yote. Hapana weusi, wala hilo giza tupu, Wawezapo kujificha watendao udhalimu. Kwani yeye hana haja ya kumfikiria mtu zaidi, ili aende mbele za Mungu ahukumiwe. Yeye huwavunja-vunja mashujaa pasina kuwachunguza, Na kuwaweka wengine mahali pao. Kwa sababu hiyo yeye huyatafiti matendo yao; Naye huwapindia usiku, wakaangamia.

 

Ayubu 36:4-5 Kwani yakini maneno yangu si ya uongo; Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe. Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote; Ana uweza katika nguvu za fahamu.

 

Ayubu 37:16 Je! Wajua jinsi mawingu yalivyowekwa sawasawa, Hizo kazi za ajabu za huyo mkamilifu wa maarifa?

 

Ayubu 42:2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.

 

Zaburi 1:6 Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea

 

Zaburu 7:9 Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki.

 

Zaburi 11:4 Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.

 

Zaburi 33:13-15 Toka mbinguni Bwana huchungulia, Huwatazama wanadamu wote pia. Toka mahali pake aketipo Huwaangalia wote wakaao duniani. yeye aiumbaye mioyo yao wote Huzifikiri kazi zao zote.

 

Ayubu 37:18 Je! Waweza kuzitandaza mbingu pamoja naye, Ambazo zina nguvu kama kioo cha kuyeyushwa?

 

Zaburi 38:9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.

 

Zaburi 44:21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.

 

Zaburi 66:7 Atawala kwa uweza wake milele; Macho yake yanaangalia mataifa; Waasio wasijitukuze nafsi zao.

 

Zaburi 73:11 Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?

 

1Wakorintho 3:20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili.

 

Kwa hiyo Mungu najaribu mioyo na mwongozo au mapenzi na hiyari ya mwanadam wanavyojitoa kwake. Kiusahihi, kuanzisha mioyoni mwao viwango vya kujitoa au kumaanisha ambavyo kwavyo watajisaidia wenyewe.

Zaburi 94:9-11 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione? Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue? Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.

 

Zaburi 119:168 Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.

 

Wateule wako mikononi mwake.

Zaburi 121:3-4 Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye; Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

 

Zaburi 139:1-24 Ee Bwana, umenichunguza na kunijua. Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali. Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.  Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana. Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako. Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia. Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa. Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu. Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana, Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi; Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado. Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake! Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe. Ee Mungu, laiti ungewafisha waovu! Enyi watu wa damu, ondokeni kwangu; Kwa maana wakuasi kwa ubaya, Adui zako wakutaja jina lako bure. Je! Bwana nisiwachukie wanaokuchukia? Nisikirihike nao wakuasio? Nawachukia kwa ukomo wa chuki, Wamekuwa adui kwangu. Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.

 

Zaburi 142:3 Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.

 

Bwana anawajua watu wake. Uelewa wake ni wa hakika.

Zaburi 147:4-5 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina. Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

 

Isaya 40:26 Inueni macho yenu juu, mkaone; ni nani aliyeziumba hizi; aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina; kwa ukuu wa uweza wake, na kwa kuwa yeye ni hodari kwa nguvu zake; hapana moja isiyokuwapo mahali pake. 

 

Mithali 15:3 Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.

 

Mithali 15:11 Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za Bwana; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?

 

Mithali 16:2 Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huzipima roho za watu.

 

Kwahiyo, Mungu anaijua mioyo ila anawajaribu. Huku ni kuanzisha mchkato wa kuelewea moyo wa kila mmoja ili waweze kuingia kwenye hukumu ya haki.

 

Mithali 17:3 Kalibuni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu; Bali Bwana huijaribu mioyo.

 

Mithali 24:12 Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?

 

Isaya 28:29 Hayo nayo yatoka kwa Bwana wa majeshi, mwenye shauri la ajabu, apitaye wote kwa hekima yake.

 

Isaya 29:15-16 Ole wao wanaojitahidi kumficha Bwana mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye? Ninyi mnapindua mambo; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu?

 

Isaya 40:13-28 Ni nani aliyemwongoza roho ya Bwana, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake? 14 Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonyesha njia ya fahamu? 15 Tazama, mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, huhesabiwa kuwa kama mavumbi membamba katika mizani; tazama, yeye huvinyanyua visiwa kama ni kitu kidogo sana. 16 Lebanoni nayo hautoshi kwa kuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa kafara. 17 Mataifa yote huwa kama si kitu mbele zake; huhesabiwa kwake kuwa duni ya si kitu, na ubatili. 18 Basi, mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani? 19 Sanamu fundi mmoja huiyeyusha, na mfua dhahabu huifunika dhahabu, huifulia mikufu ya fedha. 20 Yeye aliye maskini sana hata hawezi kutoa sadaka ya namna hii, huchagua mti usiooza, hujitafutia fundi mstadi wa kusimamisha sanamu ya kuchonga isiyoweza kutikisika. 21 Je! Hamkujua? Hamkusikia? Hamkuambiwa tokea mwanzo? Hamkufahamu tangu kuwekwa misingi ya dunia? 22 Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa; 23 ndiye awatanguaye wakuu, na kuwabatilisha waamuzi wa dunia. 24 Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu. 25 Mtanifananisha na nani, basi, nipate kuwa sawa naye? Asema yeye aliye Mtakatifu. 26 Inueni macho yenu juu, mkaone; ni nani aliyeziumba hizi; aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina; kwa ukuu wa uweza wake, na kwa kuwa yeye ni hodari kwa nguvu zake; hapana moja isiyokuwapo mahali pake. 27 Mbona unasema, Ee Yakobo, mbona unanena, Ee Israeli, Njia yangu imefichwa, Bwana asiione, na hukumu yangu imempita Mungu wangu asiiangalie? 28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki. 

 

Mungu hafanyi kazi kwa mtindo wa zamu ya masaa manane. Vitu vyote vinavyofanywa na mataifa yote yamejulikana. Watu hao wataingia kwenye hukumu ya haki kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Ni wateule peke yao ndio wanaohukumiwa sasa. Wateule wanajiunga kutoka kwenye makundi mawili. Kungi la kwanza ni lile la watu 144,000 kutoka kwenye makabila. Hiki ni kiini cha uhusiano wa kumaongozi wa Ufalme wa Mungu. Kundi la maandiko ni mkutano mkubwa wanaostahili kwa utii rahisi na imani kwa utaratibu wan je wa kimaongozi. Watakuwa wote wafalme na watawala kwa kiwango wanachostahili. Hawa watu 144,000 wanaonekana kuwa walichaguliwa kwa msingi wa watu sabini na mbili kwa kipinndi cha mwaka kwa Yubile 120. Kwa maneno mwngine ni kusema kwamba watu 3,600 wanachaguliwa kwa kila Yubile. Msingi halisi wa muundo huu imeelezewa kwenye jarida la Mavuno ya Mungu, Sadaka ya Mwandamo wa Mwezi Mpya na wale 144,000 (Na. 120). Ujuzi umeelezwa kwa hatua kama siri.

 

1Wakorintho 2:7 bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

 

Hii inafanyika kama siri ili kuwalinda wateule. Mara tu baada ya idadi kamili ya hawa 144,000 itakapotimia, ndipo siri hii itafunuliwa. Ndipo watu wote watajaribiwa. Wateule wanajulikana kwa kupitia uweza wa Mungu wa kujua kila jambo. Wateule wameitwa tangu mwanzoni.

 

1Petro 1:2 kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.

 

Isaka alikuwa ni mmoja wa wateule. Mungu alijua kuwa haendi kuuawa.

 

Isaya 41:4 Ni nani aliyetenda na kufanya jambo hilo, aviitaye vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, wa kwanza na wa mwisho, mimi ndiye. 

 

Uelewa kamili wa Mungu unawezesha roho ya unabii. Wanajulikana na kutangazwa tangu mwanzoni.

 

Isaya 42:9 Tazama, mambo ya kwanza yamekuwa, nami nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapasheni habari zake. 

 

Isaya 44:7 Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze.

 

Vitu vyote vimewekwa kwa utaratibu na Mungu, ili kwamba nyakati za mpango wa wokovu haziwezi kuuizwa au kupingwa na Malaika waasi. Hii ndiyo sababu mnara wa Babeli uliharibiwa. Ndipo ustaarabu wa uliendelea kwa kiasi kwamba ulikuwa unaendelelea, ndipo matokeo ya mwisho ulianza kuwa ni kuharibika kwa mfumo wote wa jua na huenda hata kimakundi na zaidi. Nyakati za maadui zilithibitika kwa kipindi maalumu ili kuwezesha uzidishaji wa idadi ya watu kwa mazingira mazuri sana.

 

Wakati mwingine Mungu anayaanzisha mataifa kwa kuwalinda wateule na kuueneza mpango wake kwa kina zaidi.

 

Isaya 45:4 Kwa ajili ya Yakobo, mtumishi wangu, na Israeli, mteule wangu, nimekuita kwa jina lako; nimekupa jina la sifa; ijapokuwa hukunijua (soma pia aya ya 21)

 

Mungu anautangaza mwisho tangu mwanzo. Kwa hiyo, matendo ya kila mmoja yapasa yaonekane kama mlolongo wa mawazo ya kweli mtindo au utaratibu kama wa upana wa mara vinne ya mwanzoni.

Isaya 46:10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.

 

Isaya 48:3-6 Mimi nimehubiri mambo ya kale tangu zamani; naam, yalitoka katika kinywa changu, nikayadhihirisha; naliyatenda kwa ghafula, yakatokea. 4 Kwa sababu nalijua ya kuwa wewe u mkaidi, na shingo yako ni shingo ya chuma, na kipaji cha uso wako ni shaba; 5 basi nimekuonyesha tangu zamani; kabla hayajatukia nalikuonyesha; usije ukasema, Sanamu yangu imetenda haya; sanamu yangu ya kuchonga, na sanamu yangu ya kuyeyusha, imeyaamuru. 6 Umesikia haya; tazama haya yote; nanyi, je! Hamtayahubiri? Nimekuonyesha mambo mapya tangu wakati huu, naam, mambo yaliyofichwa, usiyoyajua.

 

Mchakato huu wa Uweza wa Kujua Kila jambo au Uelewa wa Kimungu unaendelea.

 

Isaya 66:18 Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu.  

 

Kwa hiyo, mchakato huu unaendelea kwa kupitia ufufuko na hukumu. Mungu anajaribu kuburudishwa na mioyo ya watu kwa kupitia wajumbe wake chini ya Yesu Kristo.

 

Yeremia 11:20 Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki, ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu. Pia soma Yeremia 20:12.

 

Yeremia 17:10 Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.  

 

Yeremia 23:24 Je, mtu ye yote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema Bwana. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema Bwana.

 

Yeremia 32:19 mkuu wa mashauri, mweza katika kutenda; ambaye macho yake yamefumbuka juu ya njia zote za wanadamu, kumpa kila mtu kwa kadiri ya njia zake, na kwa kadiri ya matunda ya matendo yake,

 

Ufufuo wa pili wa wafu kwa hiyo unafungamanishwa na hali ya kila mmoja sawasawa na jinsi walivyoishi na kuwalivyotenda wakati wa maisha yao ya kwanza. Michakato hii inachukuliwa tabia na tabia hizo haziwezi kufichwa kwa Mungu. Roho Mtakatifu anawachunguza na kuyaona na hata kama kila mmoja hajapewa Roho kwa njia ya ubatizo. Kwa hiyo, matendo ya Roho kwa mujibu wa hali ya kujua kila jambo aliyonayo Mungu huthibitisha uweza wake wa kujua kila kitu.

 

Ezekieli 11:5 Roho ya Bwana ikaniangukia, naye akaniambia, Nena, Bwana asema hivi; Mmesema maneno hayo, Enyi nyumba ya Israeli; maana mimi nayajua yaingiayo katika mioyo yenu.

 

Yeremia 51:15 Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.

 

Hakuna wakati wowote ambao Bwana aliwahi kuisahau hii dunia. Wala hajawahi kuyasahau maovu yanayofanywa na watu. Ni mpole atendapo, kwa rehema.

Ezekieli 9:9 Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, Bwana ameiacha nchi hii, naye Bwana haoni.

 

Udhihirisho wa Mungu kwenye utoaji dhabihu ulimhusisha Isaka haushindanishwi na asili ya Mungu Baba au Eloa, lakini ingekuwa ni vizuri zaidi kwa msaidizi wa Mungu Elohim wa Israeli. Ufafanuzi zaidi mwingine ni kwamba Mungu alikuwa anamjaribu tu Ibrahimu kwa kupitia Malaika, na akijua kitakachtokea na kwamba kumjaribu kule kulikuwa ni kuwaonyesha wote wawili kwa Kristo na Ibrahimu kwamba wito na uweza wa Mungu wa kujua yote hauna makosa. Jaribu la Ibrahimu halikuwa kwamba alitakiwa amtoe mwanae wa pekee sadaka tu na ambaye kwamba ndiye aliyejumuishwa kwenye ahadi, bali ilikuwa pia ni kuanzisha aina ya imani iliyohitajika kwenye moyo au mawazoni mwa mtu na kumuonyesha Isaka na kwa hata kwa Israeli kwamba utii wake kwa Mungu ulikuwa unazingira wote. Makosa au upotoshahaji wa pili ya utoaji wa sadaka ya binadamu ulikuwa uanze kwa uendelevu mkubwa mawazoni mwa Ibrahimu.

 

Matendo ya Mungu yanakuwa yamezingirwa kama Amosi anavyoonyesha.

Amosi 9:2-4 Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko. 3 Nao wajapojificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta na kuwatoa toka huko; na wajapositirika katika vilindi vya bahari nisiwaone, nitamwagiza joka huko, naye atawauma. 4 Nao wajapokwenda hali ya kufungwa mbele ya adui zao, nitauagiza upanga huko, nao utawaua; nami nitawaelekezea macho yangu niwatende mabaya, wala si mema.

 

Danieli anaonyesha kwamba uweza huu wa kujua kila kitu hauhusiani na gawio au ukaribu. Kujua nyakati za mwisho ulijulikana tangu mwanzo na ulitangazwa na Mungu.

Danieli 2:20-28 Danielii akajibu, akasema, Na lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na uweza ni wake. 21 Yeye hubadili majira na nyakati; huuzulu wafalme na kuwamilikisha wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa; 22 yeye hufunua mambo ya fumbo na ya siri; huyajua yaliyo gizani, na nuru hukaa kwake. 23 Nakushukuru, nakuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu, uliyenipa hekima na uwezo, ukanijulisha hayo tuliyotaka kwako; maana umetujulisha neno lile la mfalme. 24 Basi Danielii akaenda kwa Arioko, aliyewekwa na mfalme kuwaangamiza wenye hekima wa Babeli; alikwenda akamwambia hivi, Usiwaangamize wenye hekima wa Babeli; niingize mimi mbele ya mfalme, nami nitamwonyesha mfalme ile tafsiri. 25 Ndipo Arioko akamwingiza Danielii mbele ya mfalme kwa haraka, akamwambia hivi, Nimemwona mtu wa hao wana wa Yuda waliohamishwa, atakayemjulisha mfalme ile tafsiri. 26 Mfalme akajibu, akamwambia Danielii, aliyekuwa akiitwa Belteshaza, Je! Waweza kunijulisha ile ndoto niliyoiona, na tafsiri yake. 27 Danielii akajibu mbele ya mfalme, akasema, Ile siri aliyoiuliza mfalme, wenye hekima hawawezi kumfunulia mfalme; wala wachawi, wala waganga, wala wanajimu; 28 lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri, naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayokuwa siku za mwisho.

 

Mungu anadhihirisha hili kwa hatua kwa kupitia manabii na wateule wanaoitwa sawasawa na kujualikana kwao tangu mwanzo na hekima yake.

 

Warumi 8:27-30 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu. 28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. 29 Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.

 

Hatutaanguka iwapo kama tumejulikana tangu mwanzo na Mungu. Yeye anayajua matendo yetu kwa uwezo wake wa kujua kila kitu. Tunajaribiwa ili kutuimarisha na kutusogoza mbele hukumuni. Kwa mchakato huu sisi tu mfano na ushuhuda kwa ulimwengu, sio tu kwa kuwaendeleza wateule. Hao wanaoanguka waliitwa tu ila hawakuchaguliwa.

 

Maandalizi ya wateule yanafanyika chini ya Malaika wa YHVH ambaye ndiye Kristo.

 

Malaika na Mke wa Isaka

Huyu mjumbe au msaidizi wa Mungu anaitwa Malaika wa YHVH, ambaye anamwangalia Ibrahimu, anaitwa kutumika wakati alipokuwa anaondoka mtumishi wa Ibrahimu na kwenda kumtafutia mke Isaka. Ibrahimu alimuita kiumbe huyu kuwa ni:

Mwanzo 24:7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya babangu, na kusema nami katika nchi niliyozaliwa, aliniapia akisema, Nitawapa uzao wako nchi hii; yeye atampeleka malaika wake mbele yako, nawe utamtwalia mwanangu mke tokea huko; Interlinear)

 

Kiumbe huyu hapa ni Yahova au YHVH, Elohim wa mbingu kwa mujibu wa SHD 8064, Shâmeh, mawingu au kiwango cha juu kinachotajwa kwenye tundu linaloonekana ambayo kwayo mawingu huondoka pia na mbingu za juu sana. Kiumbe aliyemtokea Ibrahimu alikuwa Elohim wa Israeli na siyo Eloah.

 

Kuchaguliwa kwa Ibrahimu lazima kulifanyika kwa agizo la Eloah akiutendea kazi uweza wake wa kujua kila jambo. Malaika anayetajwa hapa ni msaidizi. Hata hivyo, alichukuliwa kama kuchukua na kutendea kazi uweza na mamlaka ya Mungu.

 

Mtumishi wa Ibrahimu alisindikizwa na Malaika:

Mwanzo 24:39-40 Nikamwambia bwana wangu, Labda huyo mwanamke hatafuatana nami. Akaniambia, Bwana, ambaye naenenda machoni pake, atapeleka malaika wake pamoja nawe, atafanikisha njia yako;

 

Mtumishi anamtaja Malaika huyu kuwa ni Mungu wa bwana wake.

Mwanzo 24:42-44 Nami nikaja leo kisimani, nikasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, ukinifanikishia sasa njia yangu niendayo mimi, tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji; basi na iwe hivi, msichana ajaye kuteka maji, nikamwambia, Nipe, nakuomba, maji kidogo katika mtungi wako ninywe, naye akaniambia, Unywe wewe, na ngamia zako pia nitawatekea, huyo na awe ndiye mke Bwana aliyemwekea mwana wa bwana wangu.


 Mrejesho unaonyesha kwamba wakati alipokuwa Malaika wa YHVH kuwa alikuwa pamoja nay eye, Malaika anatajwa kuwa ni YHVH (au Yahova). Jina au Cheo chake vinaonyesha mamlaka na matumizi yake hapa yanaonyesha nadharia au imani ya Kiyahudi ya vitu vitendavyo kazi kwa usaidizi vinavyopewa majina au vyeo kwa kupewa na kuruhusiwa. Kwa hiyo, ndipo dhana ya kutenda kazi kwa kusaidia, ni sawa na kama ilifanyika kwa uweza, unaoitwa wa Mungu. Dhana yenyewe inaenea na kuzaidi kuonekana kwa maelezo ya mtumishi wake.

Mwanzo 24:48 Nikainama, nikamsujudia Bwana, nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, aliyeniongoza njiani, nimtwalie mwana wa bwana wangu binti wa ndugu yake.

 

Hitimisho la Msingi

Hitimisho ile linalojitokeza kuwa haliepukiki ni kwamba Elohim wa Ibrahimu na, ambaye ni wa Israeli, ni Malaika, ambaye ni mjumbe, kama msaidizi wa Mungu ambaye ndiye anayatenda mapenzi ya Mungu, Eloah.

 

Usaidizi, hata hivyo, hau kutoka kwenye mamlaka. Uwepo wa Malaika au mjumbe ni sawa na uwepo wa Mungu, na wa Malaika mwenyewe ni muonekano wa zama za kabla ya kuzaliwa kimwili hapa duniani kama tunavyojionea kwenye vifungu kadhaa mbalimbali. Kumuona Malaika ni kumuona Mungu, na kwa kweli, ndipo mahali ambapo kitendo cha kutembelea kinapofanyika kuwa ni kitakatifu kama ilivyokuwa huko Sinai na Musa. Dhana ya usaidizi wa huyu Elohim linaungwa mkono au kupata mashiko na maandiko.

 

Hitimisho la Pili

Huyu elohim anahusishwa na uanzishwaji wa mstari na uchaguzi wa mteule kwa msingi endelevu. Msingi wa mstari wa uzawa umefanyika ili kuweshesha uwepo wa hawa 144,000 kutka kwenye makabila, sawasawa na urithi wao. Kristo anatoa hakikisho kwamba kila mmoja amebakizwa pale ilipo muhimu kualiza mpango kama ulivyoeleweka na Mungu. Haipaswi tushindwe tuharibiwapo. Ndoa yetu ipo imara na Mwanakondo wa Mungu.

q