Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[CB33]
Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu
(Toleo
La 2.0 20030612-20070125)
Mara tatu kwa
kila mwaka Wakristo wameamriwa kutoka nje ya makazi au nyumba zao na waende
wakakusanyike pamoja mahali atakapolikalisha Bwana jina lake ili wakazishike
huko Sikukuu alizowaamuru Mungu. Idi ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu ni
maadhimisho ya kwanza kati ya Sikukuu hizi tatu.
Christian Churches of God
(Hati Miliki © 2003, 2007
Kellie Elson, ed Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu
Swali: Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa
Chachu Ni nini?
Ni
mojawapo ya Sikukuu kubwa ambazo Bwana Mungu wetu aliamuru tuziadhimishe kwa
kwenda huko kila mwaka, tunapokuwa tunakusanyika pamoja nje ya nyumba zetu na
kuyafanya yale anayotuamuru kuyafanya. Tunaukumbuka wakati huu kuwa ni ule ambao
Mungu aliwatoa wana wa Israeli kutoka utumwani Misri.
Swali: Kwa nini hatuketi majumbani
mwetu tunapoishika Sikukuu Hii ya Mikate isiyotiwa Chachu?
Kumbukumbu la Torati
16:5-6 Usimchinje pasaka
ndani ya malango yako yote akupayo Bwana, Mungu wako; 6 ila mahali atakapochagua Bwana,
Mungu wako, apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja pasaka jioni, katika
machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri
Mungu anatuambia
kwamba tusile kitu ch0chote chenye chachu au hamira wakati huu wa maadhimisho
ya Pasaka.
Kutoka 12:17-20
Nanyi mtaitunza ile sikukuu ya mikate isiyochachwa; kwa kuwa katika siku
iyo hiyo mimi nimeyatoa majeshi yenu katika nchi ya Misri; kwa hiyo mtaitunza
siku hiyo katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele. 18 Mwezi
wa kwanza, siku ya mwezi kumi na nne, wakati wa jioni, mtakula mikate
isiyochachwa, hata siku ya mwezi ishirini na moja jioni. 19 Muda
wa siku saba isionekane chachu katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote
atakayekula hiyo iliyotiwa chachu, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na mkutano wa
Israeli, akiwa mwenye kukaa hali ya ugeni, au akiwa mtu aliyezaliwa katika
nchi. 20 Msile kitu chochote kilichochachwa;
mtakula mikate isiyochachwa katika makao yenu yote
Hapa Bwana
anatuambia anatuambia kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.
Anatuambia pia wakati unaopaswa kuiadhimisha. Mwezi wa Kwanza wa mwaka mpya
unaitwa mwezi wa Abibu. Maadhimisho ya Sikukuu ya Pasaka yanaanza tangu siku ya
14 ya mwezi wakati wa jioni na inaendelea hadi siku ya 21 ya mwezi wakati wa
jioni. Hii ni Sikukuu ya siku saba na tunakusanyika katika jioni au usiku wa
siku ya 14 ili kuja kusherehekea na kuadhimisha Ushirika wa Meza ya
Bwana. Tangia siku ya 15 hadi siku ya 21 ni Siku Takatifu.
Tunazitakatifuza siku hizi sawa na kama tunavyoadhimisha na kuzitakatifuza
Sabato za kila juma. Kwa hiyo, tutakula mikate isiyotiwa chachu kabisa kwa muda
wa siku saba. Tujihadhari kutokula kitu chochote chenye chachu au hamira ndani
yake. Hamira ni mseto ili kuifanya iumuke. Hii inaashiria au dalili ya vitu
anavyovitumia Mungu ili kutufundisha kwamba sisi hatujakamilika pasipo yeye.
Hii ni namna inayoashiria dhmira ya kuondoa dhambi au kuachana na dhambi maishani
mwetu.
Tumeelekezwa ama
kuamriwa kufanya hivyo kwa vizazi vyetu vyote milele. Hii inamaanisha kuwa
wazazi wanapaswa kuiadhimisha, kisha watoto nao wanapaswa kuiadhimisha na hara
watoto wa watoto wao waendelee kufanya hivyo vizazi vyao vyote. Ni muhimu kwa
watoto kushiriki kwenye maadhimisho ya Pasaka ili wasikilize na kujifunza
yanayofanyika na kwa nini inafanyika hivyo, ili kwamba kipindi chao kikifika
wayakapokuwa watu wazima wapate kuyajua majira au wakati, sababu na sababu ya
kufanya maadhimisho haya.
Swali: Kwa nini tunaidhimisha Pasaka?
Kutoka 12:14 Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi
mtaifanya iwe sikukuu kwa Bwana; mtaifanya iwe sikukuu katika vizazi vyenu
vyote, kwa amri ya milele
Tunaiadhimisha
Pasaka kwa kuwa Bwana Mungu wetu ametuamuru kufanya hivyo.
Ukumbusho
maana yake ni kipindi tunachoakumbuka na kuadhimisha au kusherehekea kitu
fulani likiwa kama ni tukio maalumu la namna fulani. Pia katika kipindi hiki
tunakumbuka kwamba Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na baada ya siku tatu
za usiku na mchana za kuwepo kwake kaburini alifufuka kutoka kwa wafu na kwenda
kwa Baba, Mungu wa Pekee na wa Kweli (Eloa). Kumbuka kwamba dhabihu ya Yesu
Kristo iliyolewa kwa ajili ya dhambi zetu. Tunapaswa mara zote kuiadhimisha
Sikukuu hii na kuhakikisha kuwa tunawafundisha watoto wetu. Amri hii haiwezi
kusamehewa kwa anayeivunja. Mungu alituamuru kuiadhimisha Pasaka milele!
2Wafalme 23:21 Mfalme
akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa BWANA Mungu wenu, kama
ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano
Swali: Kwa nini watoto wasishiriki Mlo
wa Ushirika wa Meza ya Bwana na kwenda na wazazi wao siku hii ya usiku wa
kwanza?
Kwenye
usiku ule wa kwanza, ni wale waongofu waliobatizwa tu ambao ni watu wazima ndio
wanaotakiwa waende kuhudhuria ibada hii maalumu ambayo wataiadhimisha kwa
kuoshana miguu yao na kisha kuila Meza ya Bwana.
Yohana 13:1-17 Ilikuwa
mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati Wake wa kuondoka
ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu Wake waliokuwa
ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho. 2Wakati alipokuwa akila
chakula cha jioni na wanafunzi Wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya
moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu. 3Yesu akijua
ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka Yake na kwamba Yeye alitoka
kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu, 4hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi
Lake la nje, kajifunga kitambaa kiunoni.
5Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi Wake miguu
na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni. 6Alipomfikia
Simoni Petro, Petro akamwambia, ‘‘Bwana, je, Wewe utaninawisha mimi miguu?’’ 7Yesu
akamjibu, ‘‘Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa’’. 8Petro
akamwambia, ‘‘La, Wewe hutaninawisha miguu kamwe’’. Yesu akamjibu, ‘‘Kama
nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami’’. 9Ndipo Simoni Petro akajibu,
‘‘Usininawishe miguu peke yake, bali pamoja na mikono na kichwa pia!’’ 10Yesu
akamjibu, ‘‘Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake
wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.’’ 11Kwa kuwa Yeye
alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema, ‘Si kila mmoja
aliyekuwa safi.’ 12Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi Yake,
akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, ‘‘Je, mmeelewa nililowafanyia? 13Ninyi
mnaniita Mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana’, hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo. 14Kwa
hiyo, ikiwa Mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu,
pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi. 15Mimi nimewawekea kielelezo
kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi. 16Amin, amin,
nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala anayetumwa si mkuu kuliko
yule aliyemtuma. 17Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama
mkiyatenda.
Yesu
alifanya kitendo cha kuwaosha miguu wanafunzi wake kama mfano ili kutuonyesha
namna ya tabia tunazotakiwa kuwa nazo. Kitendo cha kuoshana miguu ni ishara ya
unyenyekevu au kujinyenyekesha. Watu wazima wanaoshana miguu kila mtu na mwenzake
kila mwaka ili kuufanya upya ubatizo wao. Baada ya kuoshana miguu ndipo tunashiriki
sasa Ushirika Mtakatifu wa Meza ya Bwana, ambao unashirikishwa ama kuliwa na
waongofu watu wazima na waliobatizwa peke yao. Kila mmoj anatakiwa kula kipande
kidogo cha mkate usiotiwa chachu ndani yake ambao unaashiria mwili na maisha ya
Yesu Kristo na kunywa kikombe kidogo cha mvinyo. Mvinyo unaashiria damu ya Yesu
Kristo. Wanafanya mambo haya ili kuonyesha heshima kwa Bwana Mungu wetu kwa kuifuata
Torati au Sheria zake, na kuonyesha kuwa wanamwamini nyeye peke yake.
Yohana 6:53-57 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin,
nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna
uzima ndani yenu. 54 Aulaye mwili wangu
na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. 55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu
yangu ni kinywaji cha kweli. 56 Aulaye mwili wangu
na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai
kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi.
Hapa Yesu anaeleza kwa nini watu wazima waongofu inawalazimu kushiriki Meza
hii ya Bwana. Kama hawataila Meza ya Bwana hawataweza kuuingia Ufalme wa Mungu.
Wanapaswa kujiandaa na kuwa tayari kwa kushiriki Meza ya Bwana kwa kuwasamehe
wengine wenye matatizo yoyote yale ambayo yamejitokeza katika kipindi chote cha
mwaka, na wanapaswa kutilia maanani pia umuhimu wa uhusiano wao na Mungu na
kusahihisha makosa na kudhamiria kutotenda tena dhambi na makosa waliyoyafanywa
mwaka uliopita.
Swali: Vihi vyakula vyenye chachu au
amira ni nini?
Angalia
jedwali letu tuliloziorodhesha picha na tangazo moja lililoorodhesha aina
mbalimbali ya vyakula na vinywaji vyenye chachu na hamira. Hili litatusaidia
kukumbuka na kuvijua vyakula na vinywaji vyote vyenye chachu au hamira na vile
visivyokuwa navyo.
Pia
angalia kwenye jarida la Siku Takatifu za Mungu (Na. CB22) [God’s
Holy Days (No. CB22)].
q